SIJABEBWA NA UVCCM BALI UWEZO WANGU NDO UMEFANYA NIPEWE NAFASI NILIYONAYO KWA SASA"JOKATE"

SIJABEBWA NA UVCCM BALI UWEZO WANGU NDO UMEFANYA NIPEWE NAFASI NILIYONAYO KWA SASA"JOKATE"


Mwanamitindo Jokate Mwegelo ambaye kwa sasa ni  Kaimu Katibu wa uhamasishaji na chipukizi wa Umoja wa vijana wa chama cha mapinduzi (UVCCM )  amekanusha uvumi unaosambaa kwenye mitandao ya kijamii nchini kuwa amepewa nafasi hiyo kwa upendeleo yani kwa kubwebwa na Mwenyekiti wa UVCCM.


"Unajua mimi nimejitoa sana kwa jamii yangu na kazi yangu inaonekana na jamii na wala siyo ya kificho hivyo nimepewa nafasi hii kutokana na kujitoa kwangu kuitumikia jamii"amesema Jokate mbele ya waandishi wa habari waliomuuliza kuhusu uvumi huo.

Katika hatua nyingine Uvccm  yawaasa vijana kujitokeza kwa wingi April 26 katika maadhimisho ya miaka 53 ya muungano mjini Dodom.


 Hayo yamesemwa jana na umoja wa vijana wa chama cha ccm Jijini Dar es salaam wakati walipokuwa wakizungumza na waandishi wa habari Ambapo akitoa maelezo hayo kaimu katibu mkuu wa jumuiya ya umoja wa vijana ccm Bwn. Shaka Hamdu Shaka Amesema kuwa wao kama vijana wanaounga mkono juhudi zote zinazotekelezwa na serikali ya awamu ya tano chini ya mwenyekiti wake Dr.John Joseph Pombe Magufuli wanapenda kuungana na watanzania wote hususani vijana wote hapa nchini kujitokeza kwa wingi katika sikukuu ya maadhimisho ya siku ya muungano


Aidha ameendelea kwa kusema kuwa kwa kuwa sherehe hizo zitafanyika katika mkoa wa Dodoma na hasa ikumbukwe kuwa ndiko kwenye makao makuu ya nchi pia makao makuu ya chama hivyo vijana wote waliopo dodoma wajitokeze kwa wingi ili kuweza kuungana na kusherehekea pamoja kwa siku hiyo ya maadhimisho ya Muungano wa Jamhuri ya Tanzania.


Ambapo ameongeza kuwa wao kama viongozi wa umoja wa vijana wa ccm(UVCCM) ni wakati wao wa kujivunia na kutembea kifua mbele na kujisifu kwa ajili ya nchi yao hivyo kwa jambo la maadhimisho ya sherehe za muungano halina aja ya kujali itikadi za vyama wala ukabila zaidi wajitokeze kwa wingi mara tu ifikapo siku hiyo ya tarehe 26.04.2017

Comments