CHUO CHA DMTA KUANZA KUTOA MAFUNZO YA UBAHARIA CHAFUNGUA DIRISHA LA UDAHILI
CHUO CHA DMTA KUANZA KUTOA MAFUNZO YA UBAHARIA CHAFUNGUA DIRISHA LA UDAHILI Dar es salaam -Chuo binafsi cha Dar es salaam Maritime Training Academy (DMTA) kimetangaza kuanza kutoa mafunzo katika fani za bahari (ubaharia)kuanzia Mwezi April 2026, hapa nchini. Hata hivyo chuo hicho kimeelezwa kuwa sehemu muhimu katika kuandaa rasilimali watu wenye ujuzi katika sekta ya uchumi wa buluu, kwa kuwapa vijana mafunzo ya ubaharia yatakayowawezesha kushiriki kikamilifu katika shughuli za kimataifa za usafirishaji wa mizigo kupitia bahari. Akizungumza kuhusu mchango wa chuo hicho,Kapteni Ken Michael Chimwejo amesema sekta ya bahari ina nafasi kubwa katika uchumi wa dunia, akibainisha kuwa takribani asilimia 90 ya mizigo yote duniani husafirishwa kupitia maji au bahari, hali inayofanya sekta hiyo kuhitaji wataalamu wengi wenye ujuzi wa ubaharia. Amesema kwa sasa kuna nchi kadhaa zinazoongoza duniani kwa kuwa na idadi kubwa ya mabaharia, zikiwemo Ufilipino, Urusi, Indonesia, ...








