D VOICE ATANGAZA KUANZA KWA MATAMASHA YAKE TANZANIA,KWANZA OIL YAMPA GARI
D VOICE ATANGAZA KUANZA KWA MATAMASHA YAKE TANZANIA,KWANZA OIL YAMPA GARI Dar es salaam- Msanii maarufu wa muziki wa singeli hapa nchini kutoka lebo namba moja ya burudani Afrika ya Mashariki WCB,D Voice Leo amekabidhiwa gari na kampuni ya Kwanza Oil ambayo ataitumia katika tour yake katika Mikoa 15 hapa nchini. Tour hiyo ambayo ameipa jina la D Voice tour 2026 itaanza katika Mikoa 10 kote nchini Tanzania na baadaye kwenda katika nchi mbalimbali Afrika Mashariki inatajwa kama tour kubwa kuwahi kufanywa na msanii wa Singeli hapa nchini. Akizungumza na waandishi wa Habari katika hafla fupi ya kukabidhiwa gari hilo iliyofanyika leo March 18,2026 Jijini Dar es salaam,msanii D Voice ameishukuru kampuni ya Kwanza Oil kwa Kudhamini matamasha yake ya muziki ambayo atayafanya hapa nchini akianzia Kanda ya ziwa katika Jiji la Mwanza huku akiahidi kutoa zawadi mbalimbali za mafuta kwa akina mama katika Kila Mkoa atakaopita. Amesema kukabidhiwa gari hilo ni ishara kwamba ka...

.jpeg)






