BROTHERS ACADEMY 'KUMFUNDISHA' BABA LEVO MASOMO YA SEKONDARI,AJIUNGA NAO
BROTHERS ACADEMY 'KUMFUNDISHA' BABA LEVO MASOMO YA SEKONDARI,AJIUNGA NAO Mbunge wa Jimbo la Kigoma mjini Revocatus Chipando maarufu kama Baba Levo ameanza rasmi masomo yake ya sekondari katika taasisi ya Brothers Academy ambapo atasoma elimu hiyo kwa kipindi cha miaka miwili. Akizungumza na waandishi wa Habari Jijini Dar es salaam mbunge huyo amesema kuwa ameamua kujiunga na Brothers Academy iliyopo Banana,Ukonga Jijini humo ili afikie ndoto zake za kupata elimu mpaka ngazi ya chuo kikuu. Nimejiunga na Brothers Academy kutokana na kwamba wana programu ya VIP ambayo unaweza kuhudumiwa mahali popote,mimi ni Mbunge,nina kazi nyingi za kuwahudumia Wananchi wa Kigoma Mjini,lakini pia natakiwa kusoma, hivyo hii shule(Brothers Academy)ina programu za kufundisha watu wa VIP kama mimi" amesema Baba Levo. Aidha ameongeza kuwa Shule ya Brother's Academy inatoa Elimu kuanzia darasa la saba,kidato cha kwanza hadi kidato cha sita kwa muda wa miaka 3,hivyo amewaomba,watu maarufu na ...







