MAFUNDI NA WAUNDAJI VIPIMO NCHINI WAASWA KUENDANA NA TEKNOLOJIA
MAFUNDI NA WAUNDAJI VIPIMO NCHINI WAASWA KUENDANA NA TEKNOLOJIA* Mkurugenzi wa Huduma za Ufundi kutoka Wakala wa Vipimo (WMA), Bw. Francis Olwero akizungumza na mafundi na waundaji wa vipimo mbalimbali wakati wa kikao kazi kilichofanyika baina yao na WMA Mkoa wa Dodoma, Februari 18, 2026 Dodoma kwa lengo la kujadiliana masuala muhimu kuhusu sekta hiyo.* Na WMA - Dodoma Mafundi wa vipimo, waundaji wa mizani pamoja na wapimaji wa matanki ya kuhifadhia mafuta ardhini wameshauriwa kuelekeza nguvu katika vipimo vya kidijitali kutokana na maendeleo ya teknolojia yanayoleta mabadiliko kila siku. Wito huo umetolewa na Mkurugenzi wa Huduma za Ufundi, Wakala wa Vipimo (WMA), Francis Olwero, wakati wa kikao kazi na mafunzo kwa kundi hilo, yaliyoandaliwa na Ofisi ya WMA Mkoa wa Dodoma na kufanyika Februari 18, 2026. Akifungua kikao kazi na mafunzo hayo, Mkurugenzi Olwero aliwaambia washiriki kuwa kukua kwa teknolojia kunailazimu sekta ya vipimo kuendana na mabadiliko yanayotokea ili kazi zien...







