Kampuni ya GF Trucks & Equipment LTD Kudhamini Tuzo ya Mchezaji Bora wa Mwezi Singida Black Stars
Kampuni ya GF Trucks & Equipment LTD Kudhamini Tuzo ya Mchezaji Bora wa Mwezi Singida Black Stars Na Thadei PrayGod Dar es Salaam, Februari 13, 2026 – Kampuni ya GF Trucks & Equipment LTD imeingia makubaliano rasmi ya kudhamini tuzo ya Mchezaji Bora wa Mwezi (Player of the Month) kwa klabu ya Singida Black Stars FC, katika hatua inayolenga kukuza na kuendeleza sekta ya michezo nchini. Akizungumza katika hafla ya utilianaji Saini wa makubaliano hayo iliyofanyika makao makuu ya kampuni hiyo yaliyoko Vingunguti Jijini Dar es salaam,Mkurugenzi wa Masoko na Biashara wa kampuni hiyo, Bw. Salman Karmali, alisema udhamini huo ni sehemu ya mchango wa kampuni katika kusaidia maendeleo ya michezo sambamba na shughuli zake za biashara. Alieleza kuwa kampuni hiyo imekuwepo kwa miaka 19 na imekuwa mdau mkubwa katika sekta ya malori na mitambo nchini Tanzania, huku pia ikishiriki katika shughuli za kijamii (CSR) ikiwemo michezo, afya na miundombinu. “...







