TMA YATANGAZA MWELEKEO WA MVUA ZA MASIKA NCHINI,YATOA TAHADHARI HIZI
TMA YATANGAZA MWELEKEO WA MVUA ZA MASIKA NCHINI,YATOA TAHADHARI HIZI Mamlaka ya Hali ya Hewa hapa nchini (TMA) imetoa rasmi utabiri wa msimu wa mvua za Masika 2026 kwa maeneo yanayopata mvua mara mbili kwa mwaka kwa kipindi Cha Mwezi Machi Hadi Mei 2026 huku mamlaka hiyo ikitoa tahadhari katika sekta mbalimbali. Akitangaza msimu wa mvua hizo mbele ya waandishi kutoka vyombo mbalimbali vya habari nchini,leo Februari 5,2026, Mkurugenzi Mkuu wa TMA na Makamu Mwenyekiti wa Jopo la Kimataifa la Sayansi ya Mabadiliko ya Hali ya Hewa na Tabianchi Dkt. Ladislaus Chan’ga alisema maeneo mengi ya nchi yanayopata misimu miwili ya mvua yanatarajiwa kupata mvua za wastani hadi juu ya wastani. “Mvua za Wastani hadi Juu ya Wastani zinatarajiwa katika maeneo mengi ya nchi ikihusisha Pwani ya Kaskazini pamoja na baadhi ya maeneo ya Magharibi mwa ukanda wa Ziwa Viktoria (mikoa ya Kagera na Geita) pamoja na kaskazini mwa mkoa wa Kigoma, isipokuwa maeneo ya Nyanda za Juu Kaskazini M...








