TUZO WA WORLD TRAVEL KUFANYIKA ZANZIBAR AGOSTI 28
ZANZIBAR KUWA MWENYEJI WA WORLD TRAVEL AWARDS KWA MARA YA KWANZA Zanzibar imepewa fursa ya kuwa mwenyeji wa tuzo za 33 za World Travel Awards , hatua inayolenga kuitangaza zaidi Zanzibar katika ramani ya utalii duniani na kuongeza fursa za uwekezaji katika sekta hiyo. Zaidi ya wageni 250 kutoka mataifa mbalimbali wanatarajiwa kushiriki katika tukio hilo, wakiwemo wawekezaji katika sekta ya hoteli pamoja na wawakilishi wa mashirika ya ndege. Akizungumza na waandishi wa Habari jijini Dar es salaam Leo Agosti 24,2026 kuhusu tukio hilo, Mwenyekiti wa Bodi ya Kamisheni ya Utalii Zanzibar, Suleiman Ali Mohamed, amesema kuwa,kuwa mwenyeji wa tuzo hizo ni fursa kubwa kwa Zanzibar kutangaza vivutio vyake vya utalii, kukuza uwekezaji na kuhakikisha wananchi wananufaika na sekta hiyo kupitia dhana ya utalii endelevu. Amesema Serikali pia inalenga kuimarisha miundombinu ya utalii ili kuwezesha kufikiwa kwa malengo ya kukuza sekta hiyo na kuongeza mchango wake katika uchumi wa Zanzibar....









