WATU 11 MBARONI KWA TUHUMA ZA WIZI WA MIUNDOMBINU YA TTCL
WATU 11 MBARONI KWA TUHUMA ZA WIZI WA MIUNDOMBINU YA TTCL DAR ES SALAAM: Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam linawashikilia watu 11, akiwemo Timothy Eshemo maarufu kwa jina la Jack, kwa tuhuma za kuiba miundombinu ya Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL). Taarifa hiyo imetolewa Agosti 27, 2026 na Kamanda wa Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, SACP Jumanne Muliro, wakati akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam. SACP Muliro amesema baadhi ya watuhumiwa hao wanadaiwa kujihusisha na kupanga uhalifu, kuiba pamoja na kununua miundombinu hiyo kwa lengo la kufanya biashara. Amesema miundombinu inayodaiwa kuibwa ni pamoja na nyaya za shaba (copper cables), ambazo zimekuwa zikisababisha kukatika au kuathiriwa kwa huduma za mawasiliano katika taasisi mbalimbali za Serikali na binafsi. “Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam linalaani hujuma hizi na litawashughulikia wale wote wanaohusika kupanga na kuiba miundombinu hiyo,” amesema SA...









