KAMATI YA UTALII, BIASHARA NA KILIMO BARAZA LA WAWAKILISHI YADHAMIRIA MAMLAKA YA VIPIMO ZANZIBAR IFIKIE VIWANGO VYA WMA BARA
KAMATI YA UTALII, BIASHARA NA KILIMO BARAZA LA WAWAKILISHI YADHAMIRIA MAMLAKA YA VIPIMO ZANZIBAR IFIKIE VIWANGO VYA WMA BARA Na Veronica Simba - WMA Kamati ya Utalii, Biashara na Kilimo ya Baraza la Wawakilishi Zanzibar, imekiri kuvutiwa na utendaji kazi wa Wakala wa Vipimo (WMA) Tanzania Bara na kuahidi kuweka mikakati ya makusudi itakayoisaidia Mamlaka inayosimamia vipimo nchini humo (ZAWEMA) kutekeleza majukumu yake kwa kiwango hicho au zaidi. Akizungumza na waandishi wa habari mapema leo Aprili 16, 2026 baada ya ziara ya mafunzo katika Kituo cha Vipimo Misugusugu, mkoani Pwani, Makamu Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Mhe. Dkt. Mohammed Ali Suleiman, amesema Wakala wa Vipimo upande wa Tanzania Bara wamepiga hatua kubwa kiutendaji hivyo kuna kila sababu ya Zanzibar kufuata mfano huo. “Tumeona wenzetu wamefanya kazi kubwa na wana vipimo vya kisasa ambavyo vinawawezesha kuhakiki mathalani kiwango cha maji anachotumia mteja ndicho anacholipia, halikadhalika kwenye umeme...







.jpeg)

