TANZANIA NI NCHI TAJIRI WAZEE WETU WALITUACHIA RASILIMALI TUZITUMIE VIZURI:SHIGONGO
Mbunge wa Jimbo la Buchosa,Mkoani Mwanza Erick Shigongo amesema rasilimali zilizopo kwa sasa nchini ni matokeo ya viongozi walikuwepo awali ambao walizitunza ili vizazi vilivyopo na vijavyo vije kunufaika. Shigongo ameyasema hayo hii Leo wakati alipokuwa akizungumza na waandishi wa Habari kando ya mkutano wa uzinduzi wa jukwaa la uzinduzi wa vijana lililoandaliwa na Halmashauri ya Jiji la Dar es salaam. Amesema Tanzania ni nchi tajiri mno na atalizungumza hilo mara nyingi na Kila siku hatoacha kusifu utajiri wa rasilimali zilizopo nchini. "wazee wetu Hawa walijua kuwa chini ya ardhi Kuna uranium,tena wakiwa vijana wakati ule walijua pia chini Kuna almasi,tanzanite,dhahabau na gesi na wakajua chini Kuna utajiri mkubwa ila baada ya uhuru lakini wakasema hatutautumia utajiri huu sisi watakuja wautumie watoto wetu" amesema Shigongo. Ameongeza kuwa Kazi ya viongozi wa wakati huo Ilikuwa ni moja tu kumuondoa mkoloni na walipofanikiwa kumuondoa nao wakafanya Kazi kwa muda na wali...





.jpeg)



