KILIBA AWATAKA VIJANA KUTOTUMIWA NA WANAOTAKA KUIHARIBU TANZANIA.
KILIBA AWATAKA VIJANA KUTOTUMIWA NA WANAOTAKA KUIHARIBU TANZANIA. Mwenyekiti wa taasisi ya mama asemewe Taifa,Geofrey Kiliba amewataka Vijana kutokushiriki katika harakati za kisiasa zinazolenga kubomoa na kudhoofisha maslahi ya vijana hapa nchini. Kiliba ameyasema hayo alipokuwa akizungumza na waandishi wa Habari Jijini Dar es salaam ambao amesema kuwa vijana ni hazina kubwa ya Taifa na endapo itarubuniwa na wanasiasa wasioitakia mema Tanzania basi inaweza kuwa na madhara makubwa. Amesema Umma wa vijana unapaswa kuelimishwa na kutobebeshwa ajenda za kuliharibu Taifa,kwani watakapoliharibu hawatakuwa na sehemu nyingine ya kukimblia. "Wamekuwa wakiwahadaa vijana eti wasiwaamini viongozi wao waliowachagua kwa taratibu na katiba ambayo imekuwa ikiaminika siku zote hivyo vijana wasikubali kuhadaika" amesema. Amesema mambo wanayoyafanya wale wanaowarubuni vijana kuingiza Taifa katika machafuko hayakubaliki na yakifumbiwa macho yanaweza kuigharimu Tanzania hivyo vijana wasidangan...









