TANZANIA BEACH LOFEGUARDS YAADHIMISHA SIKU YA KUZUIA KUZAMA,YATOA MAFUNZO KWA WANAFUNZI WENYE MAHITAJI MAALUM
Na Mwandishi wetu Dar es salaam Taasisi ya Tanzania beach lifeguard kwa kushirikiana na chama cha mchezo wa kuogelea nchini na wadau wengine wameadhimisha siku ya kuzuia uzamaji duniani huku ikijidhatiti katika utoaji elimu. Katika kuadhimisha siku hiyo inayoadhimishwa Leo Julai 25 duniani kote,taasisi hiyo imeendesha mafunzo kwa makundi mbalimbali wakiwemo wanafunzi wenye ulemavu ili kuwajengea uwezo wa kujiokoa inapotokea wamezama majini. Akizungumza na waandishi wa Habari jijini Dar es salaam Mwandaaji wa maadhimisho hayo ambaye ni Mkurugenzi wa Tanzania beach lifeguard Bi Amina Mfaume amesema maadhimisho hayo yenye kauli mbinu isemayo "mtu yoyote anaweza kuzama lakini mtu asizame" inayoashiria umuhimu wa kujiokoa na kuokoa majini. "kwa mwaka huu tumeamua kuwapa mafunzo watoto wenye mahitaji maalum kwani tunaamini wao ndio wapo kwenye risk kubwa sana kutokana na majanga ya maji ndo maana Leo tunawapa mafunzo hapa juu ya namna ya kuogelea na kujiokoa" amesema....









