CHUO CHA DMI CHASISITIZA UWEKEZAJI MKUBWA ELIMU, TEKNOLOJIA:UCHUMI WA BULUU
CHUO CHA DMI CHASISITIZA UWEKEZAJI MKUBWA ELIMU, TEKNOLOJIA,UCHUMI WA BULUU Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam Mkuu wa Chuo cha Bahari Dar es Salaam (DMI), Profesa Tumaini Gurumo, amesema Tanzania inahitaji kuongeza uwekezaji katika elimu, teknolojia, rasilimali watu na utekelezaji wa sheria ili kuhakikisha uchumi wa buluu unakuwa endelevu na unawanufaisha wananchi pamoja na Taifa kwa ujumla. Amesema hayo Septemba 9,2026 jijini Dar es salaam wakati akitoa ufafanuzi juu ya baadhi ya mambo yaliyoibuliwa katika Kongamano la Kimataifa la Tano la Uchumi wa Buluu huku akisisitiza kuwa pamoja na kuongeza matumizi ya rasilimali za bahari kwa ajili ya manufaa ya kiuchumi, ni muhimu pia kuzilinda na kuzitunza ili zisimalizike kutokana na matumizi yasiyo endelevu. “Tunatambua kwamba tunatazama matumizi bora ya maji tuliyonayo na rasilimali zake kwa faida za kiuchumi, lakini tusije tukajisahau kwamba tusipozitunza rasilimali hizi zinaweza kufikia mwisho na kuisha,” amesema Profesa Gurumo...









