UJIO WA KAGAME, RUTO AIBU KWA MAKUWADI WA KISIASA EA - MBETO
UJIO WA KAGAME, RUTO AIBU KWA MAKUWADI WA KISIASA EA - MBETO Na Mwandishi Wetu - Chama Cha Mapinduzi kimetaja ziara za Marais wa Rwanda na Kenya nchini ni majibu tosha kwa Wanasiasa na Wanaharakati uchwara, wanaojihusisha na Ukuwadi wa Kisiasa Afrika Mashariki. Hivyo basi, CCM kimewataka Wana Afrika Mashariki wote kupuuza uvumi usio na mashiko ukidai Mataifa EA hayana Uhusiano Mwema . Matamshi hayo yametamkwa na Katibu wa Kamati Maalum ya NEC Zanzibar, Idara ya Itikadi, Uenezi na Mafunzo, Khamis Mbeto Khamis ofisini kwake kisiwandui Visiwani Zanzibar. Mbeto alieleza hayo mara baada ya Marais hao kuitembelea nchi huku akieleza kuwa Uhusiano wa Tanzania kidiplomasia wa Kikanda na Kimataifa ,hautadhoofika Mbeto alisema wapo baadhi ya Wanasiasa na Wanaharakati Uchwara EA ambao uelewa wao ni hafifu katika Uongozi, Siasa na Utawala, hueneza taarifa hasi zikidai Tanzania haina Uhusiano mzuri na Nchi jirani. Alisema Tanzania itaendelea kufuata kanuni, taratibu, misingi ...









