MALOTO AONESHA MCHANGANYIKO WA KAULI YA DKT. NCHIMBI NA MWELEKEO WA RAIS SAMIA KUHUSU KATIBA
MALOTO AONESHA MCHANGANYIKO WA KAULI YA DKT. NCHIMBI NA MWELEKEO WA RAIS SAMIA KUHUSU KATIBA HOJA SI ‘KATIBA MPYA’ BALI NI MANENO ‘PAMBANENI, KOMAENI TUPATE KATIBA MPYA- MCHAMBUZI MANENO ‘KOMAENI NA PAMBANENI’ KUHUSU KATIBA YANATENGENEZA VIULIZO LUKUKI- MCHAMBUZI Uchambuzi mpya wa kisiasa kutoka kwa Mchambuzi wa masuala ya siasa nchini, Luqman Maloto Luqman Maloto, umeibua maswali mazito kuhusu dhamira na mbinu za kiuchambuzi zilizotumiwa na Makamu wa Rais wa Tanzania, Dkt. Emmanuel Nchimbi, kufuatia hotuba yake iliyotolewa Julai 24, 2026, kwenye Mkutano Mkuu wa 15 wa Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC). Katika hotuba hiyo, Dkt. Nchimbi aliwataka Watanzania, hususan "kukomaa" na "kupambana" ili kupata Katiba Mpya kabla ya fursa iliyopo kumpoteza Rais Samia Suluhu Hassan ambaye kwa mujibu wa Nchimbi, ana utashi wa dhati wa kukamilisha mchakato huo. Hata hivyo, Maloto katika andiko lake lenye kichwa "kumwelewa nchimbi inatakiwa ung’amue alik...









