MADEREVA WMA WASHIRIKI KONGAMANO LA CHAMA CHAO KITAIFA
MADEREVA WMA WASHIRIKI KONGAMANO LA CHAMA CHAO KITAIFA 🔶 WAAHIDI UTENDAJI MAHIRI ZAIDI *Na WMA - DODOMA.* Baadhi ya madereva kutoka Wakala wa Vipimo (WMA) wanashiriki Kongamano la Tano la Chama cha Madereva wa Serikali Tanzania (MST-TGDU) linaloendelea katika Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete jijini Dodoma. Kongamano hilo la kitaifa lililoanza Septemba 12 limewakutanisha mamia ya madereva wa Serikali kutoka mikoa yote nchini, ambapo pamoja na mambo mengine wanajadili mustakabali wa taaluma yao, changamoto wanazokutana nazo barabarani na namna ya kuimarisha nidhamu na weledi kazini. Kwa mujibu wa waandaaji, kongamano hili ni zaidi ya mkutano wa kawaida; ni darasa huru la kubadilishana uzoefu, kujifunza mbinu mpya za uendeshaji salama, matunzo ya vyombo vya moto vya Serikali na umuhimu wa uwajibikaji katika kulinda mali za umma. Akizungumza kwa niaba ya madereva wa WMA, Dereva Mkuu kutoka WMA Mkoa wa Dodoma, Bw. John Jumbe amesema ushiriki wao umewapa fursa ya ...









