KONGAMANO LA NNE LA KIMATAIFA LA UVUVI NA UKUZAJI VIUMBE HAI LAFUNGULIWA DAR
KONGAMANO LA NNE LA KIMATAIFA LA UVUVI NA UKUZAJI VIUMBE HAI LAFUNGULIWA DAR Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Balozi Dkt. BashirAlly Kakurwa Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Uvuvi Tanzania (TAFIRI) Dkt. Isamel Kimirei Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Balozi Dkt. BashirAlly Kakurwa, leo Agosti 24, 2026 amefungua Kongamano la Nne la Uvuvi na Ukuzaji Viumbemaji (4tFAR4ViBE) linalowakutanisha Wanasayansi, watafiti na wadau wa uvuvi na wakuzaji viumbe maji na wataalam wa vyuo vikuu kutoka katika Nchi 17 ikiwemo mwenyeji Tanzania kujadili kuhusu maendeleo endelevu ya sekta ya uvuvi na ukuzaji viumbe maji na kuweka wazi kiwa sekta ya uvuvi zinahitaji sayansi na tafiti ili kuwanufaisha wavuvi. Kongamano hilo linalofanyika kwa siku tatu katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere International Convetion Center (JNICC) Mhe. Balozi Dkt. Bashiru amewasisitiza wataalam hao kutumia kongamano hilo kujadili kwa kina jinsi ya kutumia sayansi na tafiti kwa ajili ya uvuvi endelevu na ukuza...









