MAONESHO YA ADORABLE WEDDING TRADE FAIR 2026 KUFANYIKA APRILI 17–19 EACLC UBUNGO
MAONESHO YA ADORABLE WEDDING TRADE 2025 FAIR KUFANYIKA APRILI 17–19 EACLC UBUNGO Na Mwandishi Wetu DAR ES SALAAM – Mkurugenzi Mtendaji wa Adorable Wedding Trade Fair, Anna Lema , ametangaza kufanyika kwa maonesho maalum ya biashara yanayowakutanisha watoa huduma mbalimbali za sherehe na harusi kuanzia Aprili 17 hadi 19 mwaka huu. Akizungumza kuhusu maandalizi ya tukio hilo, Anna amesema maonesho hayo yataleta pamoja watoa huduma wa sekta ya harusi ikiwemo waandaaji wa shela za harusi, watengenezaji wa keki, wabunifu wa mavazi ya harusi na huduma nyingine zinazohusiana na maandalizi ya sherehe. Amesema maonesho hayo yatafanyika katika soko la kimataifa la Afrika Mashariki EACLC lililopo Ubungo jijini Dar es salaam Amesema katika maboresho ya mwaka huu, watoa huduma watatumia fremu za maduka zilizopo ndani ya jengo husika kama mabanda ya kuoneshea bidhaa na huduma zao, hatua ambayo imepunguza gharama za maandalizi ukilinganisha na awali ambapo walilazimika kukodisha mab...









