SBL YAJA NA VIN NKOLOMBOKA,SULUHISHO LA WANAUME
Kinywaji kipya cha Vin Nkolamboka kimezinduliwa rasmi jijini Dar es Salaam katika hafla iliyohusisha wadau mbalimbali wa biashara, sekta ya vinywaji pamoja na wageni waalikwa. Uzinduzi huo umefanyika kwa lengo la kukitambulisha kinywaji hicho katika soko la Tanzania na kutoa chaguo jipya kwa watumiaji wa vinywaji vyenye kilevi. Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Meneja Mkuu wa kinywaji hicho, Domivic Salamba, amesema kuwa Vin Nkolamboka ni bidhaa mpya iliyobuniwa kwa kuzingatia mahitaji ya soko la ndani na ladha ya Watanzania. Amesema kampuni yao imewekeza katika ubora wa bidhaa hiyo ili kuhakikisha inakidhi viwango vya kitaifa na kimataifa. Salamba ameeleza kuwa kinywaji hicho kina kiwango cha kilevi cha asilimia 16, hivyo kimeidhinishwa kutumiwa na watu wenye umri wa kuanzia miaka 18 na kuendelea, kwa mujibu wa sheria na kanuni za nchi. Amesisitiza umuhimu wa matumizi ya kinywaji hicho kwa uwajibikaji ili kuepuka madhara yanayoweza kusababishwa na matumizi kupita kiasi. Ameongeza ku...







