MCHANGE AILIPUA CHADEMA/ AWATAKA WAACHE KUPOTOSHA
MCHANGE AILIPUA CHADEMA/ AWATAKA WAACHE KUPOTOSHA Habibu Mchange ameibuka na madai mazito dhidi ya viongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), akiwatuhumu kuhusika katika vitendo vya utekaji, mateso na mauaji ya vijana wasio na hatia pamoja na kupanga matukio mbalimbali ya kisiasa tangu mwaka 2011 kwa lengo la kuipotosha jamii na kuichafua taswira ya Serikali. Kwa mujibu wa Mchange, matukio hayo yanajumuisha vurugu za Arusha, tukio la Morogoro alikofariki mwanahabari Arizona, kifo cha Daud Mwangosi Iringa, madai ya kutekwa na kuteswa kwa Yona Temeke, shambulio la tindikali dhidi ya Musa Tesha, pamoja na madai ya kuteswa kwa Mkurugenzi wa Jambo Media Group Bagamoyo. Aidha, Mchange ametoa tuhuma za ulaji wa michango ya umma akidai kuwa viongozi wa Chadema wakiongozwa na John Heche waliinisha michango kwa ajili ya Mwenyekiti wa chama hicho, Tundu Lissu, ambapo shilingi milioni 41 zilipatikana lakini kwa umma ikatangazwa milioni 26 pekee. Amesema shilingi mil...








