MATUMIZI YA MBOLEA YATAJWA NA TFC KAMA CHACHU YA UPATIKANAJI WA CHAKULA NCHINI
MATUMIZI YA MBOLEA YATAJWA NA TFC KAMA CHACHU YA UPATIKANAJI WA CHAKULA NCHINI Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Mbolea Tanzania (TFC), Samuel A. Mshote, amesema matumizi ya mbolea nchini yameendelea kuongezeka na kuchangia kupungua kwa changamoto kwa wakulima pamoja na kuimarika kwa usalama wa chakula nchini. Akizungumza na waandishi wa habari katika Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba), Julai 5, 2026, Mshote alisema hali ya uzalishaji wa chakula imeendelea kuimarika, ambapo kwa sasa Tanzania inajitosheleza kwa chakula kwa zaidi ya asilimia 124, na mafanikio hayo yanatokana na juhudi za Serikali katika kuhakikisha matumizi ya mbolea yanaongezeka nchini, hali iliyosaidia kuongeza tija katika sekta ya kilimo. Mshote alisema matumizi ya mbolea yameongezeka kutoka takribani tani 360,000 kwa miaka mitatu iliyopita hadi zaidi ya tani milioni 1.2 kwa mwaka kwa mbolea aina mbalimbali zinazotumika na wakulima nchini, elimu kuhusu matumizi ya mbolea kwa wakul...








