Hakikisheni gesi yenu inapimwa kabla ya kununua – Kihulla
Hakikisheni gesi yenu inapimwa kabla ya kununua – Kihulla Na Veronica Simba - WMA DODOMA - Afisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Vipimo (WMA), Bw. Alban Kihulla amewaambia Waheshimiwa Wabunge kuwa WMA hufanya uhakiki wa mitungi ya gesi ya kupikia inayouzwa nchini ili kujiridhisha kuhusu ujazo wake kabla ya kuingia sokoni. Akizungumza katika semina kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara, Kilimo na Mifugo kuhusu majukumu ya Wizara ya Viwanda na Biashara na Taasisi zake iliyofanyika Mei 13, 2026 Bungeni Dodoma, Kihulla alisisitiza kuwa jukumu la WMA ni kuhakiki na kusimamia usahihi wa vipimo katika sekta zote, ikiwemo nishati. Hata hivyo amewahimiza wananchi wakiwemo wabunge kuchukua tahadhari zaidi wakati wa kununua gesi. “Kabla ya kununua gesi, hakikisheni mtungi huo unapimwa na muuzaji mbele yenu ili kujiridhisha kuhusu ujazo wake. Epukeni kununua gesi kutoka kwa wauzaji wasio na mizani, kwa sababu hutaweza kujua kama gesi uliyonunua ina ujazo sahihi kama ilivyoandikw...









