WATANZANIA WATAKIWA KUWAKATAA WANAHARAKATI WALIOCHOCHEA VURUGU OKTOBA 29,WALILIPWA NA MABEBERU
Watanzania wameaswa kuacha kusikiliza wanaharakati na wanasiasa wanaochochea vurugu na uvunjifu wa amani nchini, kwa kuwa watu hao hawana nia njema kwa taifa. Rai hiyo ilitolewa leo, Juni 4, 2026, jijini Dar es Salaam na mwanafalsafa wa Pan-Afrika kutoka Zimbabwe, Dk. Joshua Maponga, wakati wa mkutano na waandishi wa habari uliohusu uzinduzi wa makala inayozungumzia matukio yaliyojitokeza kabla na baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025. Makala hiyo imeandaliwa na kampuni ya African Spear Head Media. Dk. Maponga alisema kuwa baadhi ya mashirika yasiyo ya kiserikali (NGOs) yamekuwa yakipokea fedha kutoka mataifa ya nje kwa lengo la kuhamasisha vitendo vinavyokwenda kinyume na maadili na amani ya nchi, ikiwemo vurugu na migawanyiko kati ya wananchi na viongozi wao. Alisema hali hiyo ni hatari kwa ustawi na usalama wa taifa, hivyo akashauri Serikali kuchukua hatua za kufanya uhakiki wa mashirika hayo ili kubaini vyanzo vya fedha wanazopata na namna zinavyotumika. Aidha, alieleza k...








