SIKU YA USALAMA NA AFYA KAZINI APRILI 28 KUANGAZIA USTAWI WA WAFANYAKAZI
SIKU YA USALAMA NA AFYA KAZINI APRILI 28 KUANGAZIA USTAWI WA WAFANYAKAZI Serikali imesema maadhimisho ya Siku ya Usalama na Afya Mahali pa Kazi Duniani mwaka huu yataweka mkazo katika afya ya akili kazini, ikiwa ni sehemu ya juhudi za kupunguza ajali, magonjwa na vifo vinavyotokana na shughuli za kikazi. Akizungumza na waandishi wa habari kuelekea kilele cha maadhimisho hayo, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Ajira na Mahusiano Kazini), Deus Clement Sangu, amesema lengo ni kuongeza uelewa na kuhamasisha uboreshaji wa mazingira ya kazi nchini. Amesema maadhimisho hayo yalianza kuadhimishwa rasmi mwaka 2004 na kwa mwaka huu yatafanyika kitaifa mkoani Njombe, yakiratibiwa na Serikali kupitia Wakala wa Usalama na Afya Mahali pa Kazi (OSHA) kwa kushirikiana na wadau wa utatu ambao ni Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi (TUCTA), Chama cha Waajiri Tanzania (ATE) pamoja na Shirika la Kazi Duniani (ILO). Kwa mujibu wa Waziri huyo, kauli mbiu ya mwaka huu ni “Mazingira Bora ya Kaz...









.jpeg)