JAFO AWATAKA WAISLAMU KUWATHAMINI WALIMU WA MADRASA,AWAPA MOTISHA
Na Mwandishi wetu, Dar es salaam Mbunge wa Jimbo la Kisarawe ambaye pia ni mlezi wa taasisi ya Asw-Haabul Kahfi Islamic Center Dkt Seleman Jafo amewataka waumini wa dini ya kiislamu kuwajali walimu wa madrasa kwani wanajitolea kuwajengea misingi Bora watoto wao. Jafo ameyasema hayo katika mashindano ya 11 ya kuhifadhi Quran tukufu yaliyoandaliwa na Kituo hicho na kufanyika March 7,2026 katika ukumbi wa Paradise Yombo dovya Wilayani Temeke jijini Dar es salaam huku mamia ya waumini wa dini ya kiislamu wakihudhuria. Amesema walimu wa madrasa wanafanyia Kazi kubwa katika mafundisho hasa ya kitabu kitakatifu Cha Quran hivyo wazazi wanatakiwa kuwakumbuka walimu hao kwani wengi wao wamekuwa wakiishi mazingira magumu. "hakuna malipo yanayofanana kwa Ile Kazi mnayoifanya walimu wa madrasa kwa Ile Kazi ya mwenyezi Mungu na Allah awalipe kwa wingi wa wema kwa jambo hili mnalolifanya kwa vijana wetu Mungu atuingize katika pepo yake Walimu wa madrasa hawana maisha mazuri hivyo wanatakiw...








