UWEKEZAJI MKUBWA ULIOFANYWA NA SERIKALI KITUO CHA GESI ASILIA MLIMANI WALETA NAFUU KWA WANANCHI
UWEKEZAJI MKUBWA ULIOFANYWA NA SERIKALI KITUO CHA GESI ASILIA MLIMANI WALETA NAFUU KWA WANANCHI *Kituo kina uwezo wa kujaza gesi asilia kwenye magari na bajaji 800 kwa siku *Mhe. Salome Makamba ahamasisha Sekta binafsi kuwekeza katika eneo la gesi asilia *Mikoa ya Morogoro, Dodoma, Arusha, Kilimanjaro na Tanga kufikiwa na vituo vya gesi asilia NA MWANDISHI WETU Naibu waziri wa Nishati Mhe.Salome Makamba ameeleza kuwa, Serikali imefanya uwekezaji mkubwa katika kujenga kituo cha kujaza gesi asilia kwenye vyombo vya usafiri katika eneo la Mlimani jijini Dar es Salaam ambapo zaidi ya sh.Bilioni 12 zimetumika kukamilisha kituo hicho chenye uwezo wa kuhudumia magari madogo na bajaji 800 kwa siku. Mhe.Salome amebainisha hayo Novemba 12, 2025 Jijini Dar es Salaam wakati wa ziara yake ya kukagua kituo hicho kinachosimamiwa na Kampuni Tanzu ya Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania(TPDC) ya GASCO. Mhe. Salome ameeleza kuwa Serikali ya Tanzania inayoongozwa na Mhe. Dkt. Samia ...

