TAWA YAPOKEA TUZO KUTOKA KWA TAASISI YA FOUNDATION FOR DISABILITIES HOPE (FDH)
TAWA YAPOKEA TUZO KUTOKA KWA TAASISI YA FOUNDATION FOR DISABILITIES HOPE (FDH) Na mwandishi wetu, Morogoro. Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA) imepokea Tuzo ya shukrani kutoka kwa Taasisi isiyo ya Serikali inayojulikana kama Foundation for Disabilities Hope (FDH) iliyopo Mkoani Dodoma. Akizungumza katika utoaji wa tuzo hiyo iliyofanyika Julai 14,2025, katika Ofisi za Makao Makuu ya TAWA zilizopo Mkoani Morogoro, Kaimu Kamishna wa TAWA, Mlage Kabange alisema TAWA imekuwa ikishirikiana na FDH katika utoaji wa elimu kwa jamii kuhusu masuala ya uhifadhi kwa kuhamasisha jamii kuhusu umuhimu wa kuilinda rasilimali ya wanyamapori na utunzaji wa mazingira katika maeneo ya hifadhi. Sambamba na hilo, Kamishna Kabange alisema katika kuhakikisha jamii inanufaika na shughuli za uhifadhi, TAWA imeweka utaratibu maalumu wa kuruhusu wananchi kufanya shughuli za uvuvi na ufugaji nyuki katika baadhi ya maeneo inayosimamia ili kuruhusu wananchi kujipatia kipato kutoka katika ...