MWANAMKE AOLEWA NA KANISA KISA MUMEWE NI.....................

MWANAMKE AOLEWA NA KANISA


Irene Matete kutoka Matete aliwaacha wengi vinywa wazi baada ya kuoa kanisa - Mwanamke huyo alikuwa na timu yote ya Bi harusi akikiri kuolewa na kanisa, mbele ya waumini zaidi ya 200.





.Mwanamke mmoja kutoka Maseno, kaunti ya Kisumu nchini Kenya amewaacha wengi vinywa wazi baada ya kuolewa na kanisa kwenye harusi iliyokuwa na zaidi ya waumini mia mbili.

Kwa mujibu wa mtandao mmoja nchini Kenya  imefahamika kuwa Matete aliamka asubuhi na kuvalia nguo nyeupe, kama ile tu ya bi harusi kabla ya kuelekea kanisani na in Alezwa kuwa katika harusi hiyo pasta John Ngayi ambaye alifungisha harusi hiyo alimwuliza bi harusi Huyo maswali kama Yale waulizwao bwana na bibi.

Kwa mujibu pia wa Matete ni heri kuolewa na kanisa kuliko kuendelea kuishi na mumewe walioona mwaka 1979 Bw ALEMBU kutokana na bwanake huyo kuwa mlevi wa kupindukia yaan kuoelewa na pombe.



"Kwa heshima ya watoto wangu na walichokiona nikipitia,niliamua kutoolewa tena na mwanaume na kuchagua kanisa"alisema Matete.

Akiunga mkono wazo la matete,Samuel olukano ahuamua   ni Jamaa wa karibu wa mume wa Matete amesema kuwa nduguye alikuwa akimchapa kila Siku mwanamama huyo pindi akiwa amelewa.
 Kulingana na sheria za kanisa la pentecostal assemblies of God la nchini humo MTU anafaa kufunga ndoa ili kuidhinishwa kuwa kiongozi wa kanisa na kwa sababu Bi Matete alitaka kuwa kiongozi hatua yake ilikubaliwa.

Kulingana na mchungaji Ngayi harusi za namna hiyo hufanywa kwa wale ambao huamua kusahau ndoa zao za hapo awali na kuwa waaminifu daima kwa kanisa.















Comments