WAZIRI TIZEBA AWATAKA WATENGENEZAJI NA WASAMBAZAJI W MBOLEA KUTOA ELIMU KWA WAKULIMA.

Waziri wa KILIMO,Mifugo na Umwagiliaji Dr.Charles Tizeba amewataka wadau wa mbolea kuhakikisha wanatoa ushirikiano kwa wakulima kwa kutoka elimu ya namana ya matumizi bora ya mbolea kulingana na sina ya udongo.

Akizungumza wakati wa  ufunguzi wa mkutano w pili uliyowakutanisha wadau wa mbolea Dr.Tizeba amesema kuwa kuna wakulima hadi sasa hawajawahi kuona wala kushika mbolea wakati wa sgughuli zao za KILIMO hivyo wadau wa mbolea hususani makampuni yanayosambaza na watafiti mbalimbali wa masuala ya kilimo washirikiane na serikali katika kuwasidia wakulima kwa matumizi ya mbolea.
Aidha amesema kuwa serikali imefuta tozo mbalimbali katika ekta ndogo ya mbolea ili kusaidia wakulima na wafanyabiashara wa mbolea kunufaika kwa pamoja ili kuleta maendeleo katika maisha ya wakulima.

Amesema kuwa serikali itaendelea kuchukua hatua stahiki kwa wafanyabiashara ambao watakiuka maekekezo ya bei ya serikali kwa kuuza mbolea kwa gharama kubwa huku serikali imeondoa baadhi ya kodi.
"Asilimia 65 ya watanzania ni wakulima,tunataka tuone maisha ya wakulima huko vijijini yanabadilika,hivyo shughuli yenu hapa nikuwaza namna yakumbadilisha  mkulima wa Tanzania
"Alisisitiza Dr.Tizeba.

Kwa upande wake Mkuu wa shirika la maendeleo ya kijani katika kilimo barani Afrika(AGRA) Bw .Nuhu Hatibu amemkabidhi Dr.Charles Tizeba kitabu cha utafiti wa masuala yanayomkwamisha mkulima kutumia mbolea na namna ya kukabiliana na changamoto hizo,ambapo utafiti huo umefanywa na shirika hilo katika nchi zaidi ya11 barani afrika ikiwemo Tanzania.

Akizungumza mmoja wa wadau wa sekta ya mbolea Afisa masoko kutoka kiwanda cha mbolea cha minjingu Project Amosi amesema kuwa wamefurahishwa na nia ya serikali yakuhakikisha inaweka mikakati mizuri ya kuboresha sekta ya kilimo kwa kuhakikisha mbolea inazalishwa kwa wing na kuuzwa kwa bei nafuu.

Mkutano huo una malengo makubwa ya kujadili namna ya kuongeza matumizi ya mbolea,upatikanaji wa mbolea,bei nafuu ya mbolea atakayoweza kuimudu mkulima pamoja na teknolojia za kisasa katika kuendeleza sekta ya kilimo.
MWISHO




Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi, Dkt. Charles Tzeba akiongea na wadau wa Mbolea wa Tanzania alipofungua mkutano wao katika ukumbi wa mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere Dar es Salaam. 
Mkuu wa Shirika la Mapinduzi ya Kijani Afrika (AGRA) kwa Tanzania, Rwanda na Uganda, Profesa Nuhu Hatibu (kulia) akimkabidhi Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi, Dkt. Charles Tzeba zawadi ya kitabu wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa wadau mbolea walipkutana jijini Dar es Salaam Septemba 28 2017. Kutoka kushoto ni Mwenyekiti wa Umoja wa Wauza Mbolea Tanzania, Salum Mkumba na Mkurugenzi Mkazi wa Taasis ya Biashara za Mbolea Afrika (AFAP), Dkt. Mbette Mshindo. 

Mkurugenzi Mkazi wa Taasis ya Biashara za Mbolea Afrika (AFAP), Dkt. Mbette Mshindo akiongea na wadau wa mbolea wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa wadau mbolea walipokutana jijini Dar es Salaam  Septemba 28 2017. Kutoka (kushoto) ni Mwenyekiti wa Umoja wa Wauza Mbolea Tanzania, Salum Mkumba, Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi, Dkt. Charles Tzeba na Mkuu wa Shirika la Mapinduzi ya Kijani Afrika (AGRA) kwa Tanzania, Rwanda na Uganda, Profesa Nuhu Hatibu. 

Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi, Eng. Mathew Mtigumwe akitambulishwa kwa wadau.

Wadau wa Mbolea wa Tanzania  wakifuatilia mada katika mkutano wao Dar es Salaam.

Wadau wa Mbolea wa Tanzania  wakifuatilia mada katika mkutano wao Dar es Salaam.

Wadau wa Mbolea wa Tanzania  wakifuatilia mada katika mkutano wao Dar es Salaam.

Mkuu wa Shirika la Mapinduzi ya Kijani Afrika (AGRA) kwa Tanzania, Rwanda na Uganda, Profesa Nuhu Hatibu akiongea na wadau wakati wa ufunguzi wa Mkutano walipokutana jijini Dar es Salaam leo Septemba 28 2017. Kutoka (kushoto) ni Mwenyekiti wa Umoja wa Wauza Mbolea Tanzania, Salum Mkumba na Mkurugenzi Mkazi wa Taasisi ya Biashara za Mbolea Afrika (AFAP), Dkt. Mbette Mshindo na Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi, Dkt. Charles Tizeba.

Wadau wa Mbolea wa Tanzania  wakifuatilia mada katika mkutano wao Dar es Salaam.

Wadau wa Mbolea wa Tanzania  wakifuatilia mada katika mkutano wao Dar es Salaam.

Wadau wa Mbolea wa Tanzania  wakifuatilia mada katika mkutano wao Dar es Salaam.

Wadau wa Mbolea wa Tanzania  wakifuatilia mada katika mkutano wao Dar es Salaam. 

Wadau wa Mbolea wa Tanzania  wakifuatilia mada katika mkutano wao Dar es Salaam.

Wadau wa Mbolea wa Tanzania  wakifuatilia mada katika mkutano wao Dar es Salaam.

Wadau wa Mbolea wa Tanzania  wakifuatilia mada katika mkutano wao Dar es Salaam.

Wadau wa Mbolea wa Tanzania  wakifuatilia mada katika mkutano wao Dar es Salaam.

 Mkuu wa Shirika la Mapinduzi ya Kijani Afrika (AGRA) kwa Tanzania, Rwanda na Uganda, Profesa Nuhu Hatibu (kushoto)  akiteta Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi, Eng. Mathew Mtigumwe wakati wa ufunguzi wa Mkutano walipokutana jijini Dar es Salaam  Septemba 28 2017. 


Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi, Dkt. Charles Tzeba (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na washiriki wa mkutano huo katika ukumbi wa mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere Dar es Salaam.

Comments