Watoto 20 wenye matatizo ya moyo wafanyiwa upasuaji bila kufungua kifua [JKCI]Muhimbili.



DAR ES SALAAM
Watoto 20 wenye matatizo ya moyo wafanyiwa upasuaji bila kufungua kifua [JKCI]Muhimbili.









Taasisi ya moyo ya Jakaya kikwete kwa kushirikiana na taasisi ya okoa moyo wa mtoto{save a child heart-SACH] ya nchini Israel kwa watoto 20 wenye matatizo ya moyo.

Mkurugenzi wa tiba wa taasisi hiyo dkt Peter Kisenge amesema leo jijini Dar es salaam kuwa upasuaji huo unatumia mtambo wa cathlab umefanyika katika kambi maalum ya matibabu ambayo inamalizika kesho kwa kuziba matundu kwenye moyo na kutanua mishipa ya moyo.

‘’katika kambi hii tunatarajia kufanya uchunguzi kwa watoto 100 kati ya hao watoto 60 ambao watakuwa na matatizo makubwa watapelekwa nchini Israel kwa ajili ya kufanyiwa upasuaji wa kufungua kifua mwakani na watoto 40 watatibiwa hapa nchini’’amesema dkt kisenge.
Aidha kwa upande wake mkurugenzi wa taasisi ya save a childs heart,Simon Fisher amesema taasisi hiyo imekuwa ikishirikiana na taasisis ya moyo ya jakaya kikwete kwa miaka kadhaa sasa na kuwawezesha madaktari mbali mbali kwenda nchini Israel kujifunza namna ya kufanya upasuaji wa moyo huku akiishukuru taasisi hiyo kukubali kushirikiana nao kuokoa watoto wenye matatizo ya moyo hapa nchini.

Hata hivyo taasisi ya moyo ya jakaya kikwete itakuwa na kambi nyingine hapo kesho kwa watoto na watu wazima ambayo itafikia tamati November 27 mwaka huu kwa kushirikiana na taasisis ya open heart international ya nchini Australia.

Comments