Mtanzania liyeshinda taji la dunia la urembo awasili nchini,apokelewa kwa shangwe



Mtanzania aliyeshinda taji la dunia la urembo awasili nchini,apokelewa kwa shangwe


Miss worrld universiy afrika akiwa aliyevaa taji akiwa na katibu mtendaji wa baraza la sanaa la taifa BASATA,Charles Ngereza  aliyevaa shati la kitenge kulia pamoja na ndugu zake mara baada ya kuwasili nchini.



Tanzania imeingia Katika headines tena duniani mara baada ya mtanzania kuchukua taji la dunia Katika mashindano ya miss world university yaliyofanyika nchini Cambodia.


Mrembo huyo wa kitanzania QUEEN ELIZABETH MAKUNE ambaye ni mtanznia wa kwanza kuchukua taji hilo amerejea leo nchini Katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius nyerere international airport ambapo alilakiwa na mamia ya watanzania wakiwemo ndugu,jamaa na marafiki  ambao walionyesha furaha zao pindi mrembo huyo lipoingia nchini.

Awali akizungumza mara baada ya kuwasili na ndege ya shirika la ndege la Emirates QUEEN ELIZABETH amewaambia wanahabari kuwa kujiamini kwake ndiko kulimfanya kushinda taji hilo la WORLD MISS UNIVERSITY AFRICA [Continenta queen of Africa] Katika masuala ya amani ambalo warembo kutoka nchi mbali mbali  duniani walikuwa wakilishindania.

Mlimbwende huyo ameongeza kuwa atakuwa balozi mzuri wa amani Katika bara la afrika na kuiwakilisha vyema bendera ya Tanzania Katika nchi za afrika.



Naye katibu mtendaji wa baraza la sanaa la Taifa ngereBw Charles Ngereza akizungumza kwa niaba ya waziri wa habari,utamaduni,sanaaa na michezo amesema serikali imefurahishwa na ushindi wa mlimbwende huyo ambaye ameiletea sifa kubwa nchi ya Tanzania na itahakikisha inashirikiana naye hasa Katika sauala amani  

kwa upande wake mratibu wa mashindano hayo kwa hapa nchini aiyejitambulisha kwa jina la Frank amewaambia wana habari kuwa kampuni yake itaendelea kushiriki Katika mashindano hayo na itahakikisha mataji mengi kama hayo yanakuja hapa nchini.

Hata hivyo kwa upande wake mama mzazi wa mrembo huyo wa dunia na afrika ESTER JOHN KILOBA amesema amepata furaha mara baada ya binti yake kushiriki mashindano hayo na kushinda huku akiwataka wazazi ambao wanaona mashindano ya urembo kuwa ni uhuni kuachana na dhana hiyo.


QUEEN ELIZABETH MAKUNE ambaye ni mwanafunzi wa chuo kikuu cha Tanzania Institute of Accoutance  [TIA] amekuwa ni mtanzania wa kwanza kushinda taji hilo Katika bara la afrika na kuifanya Tanzania kujitangaza vyema kimataifa Katika tasnia ya ulimbwende yaliyohusisha nchi mbali mbali duniani  ukiachana na Nancy Sumary aliyeshinda taji linalofanana na hilo miaka kumi iliyopita 

Comments