Wolper: Sijawahi Kutambulisha Mwanaume Kwetu, Tunafanya Mapenzi Kujifurahisha Tu

Wolper: Sijawahi Kutambulisha Mwanaume Kwetu, Tunafanya Mapenzi Kujifurahisha Tu

SeeBait
Staa wa Bongo Movie, Jacqueline Wolper amefunguka na kusema hajawahi kumpeleka mwanaume yeyote nyumbani kwao kumtambulisha licha ya kuwa kwenye na mahusiano na wanaume tofauti kwa nyakati tofauti tangu kuwa staa.

Wolper ameanika hayo wakati akifanya interview na Global TV Online usiku wa kuamkia leo katika shoo yake ya House of Stylish iliyofanyika katika Ukumbi wa High Spirit Lounge, jijini Dar es Salaam.

Diva huyo wa filamu ambaye amewahi kukiri mwenyewe kubanjuka na mastaa wakiwemo wa Bongo Fleva alisema mastaa wengi wanafanya mapenzi kujifurahisha tu wala si kwa ajili ya kutengeneza familia ama ndoa.

“Kwa kuwa nafanya vitu vya kijamii naepukana na baadhi ya mambo, mahusiano ya mnayoyaona kwenye mitandao ni kujifurahisha tu, ndo maana najiachia, lakini mama yangu angeuwa anatumia mitandao nisingejaribu kufanya hivyo, lazima niwaheshimu wazazi wangu.

“Sijaolewa na hamna aliyepeleka mahali nyumbani kwetu, kwa nini nimtambulshe mwanaume? Siwezi!” alisema Wolper.

Comments