FMJ HARDWARE YAZINDUA PROGRAME UUZAJI WA VIFAA VYA UJENZI,MTANDAONI


FMJ HARDWARE YAZINDUA PROGRAME UUZAJI WA VIFAA VYA UJENZI,MTANDAONI


Na mwandishi wetu.




Dar es salaam
Kampuni ya usambazaji na uuzaji wa vifaa vya ujenzi [FMJ]ya jijini Dar es salaam leo imezindua programe yake ya uuzaji wa vifaa vya ujenzi kupitia mitandao mbalimbali ya kijamii ili kuwawezesha wananchi kupata huduma hiyo kwa haraka na kwa wakati zaidi.

Akizungumza na wanahabari katika hafla ya uzinduzi huo meneja mauzo wa kampuni hiyo Fredrick Sanga amesema kuwa njia hiyo itarahisisha upatikanaji rahisi wa vifaa vya ujenzi kwa wakaazi wa jiji la Dar es salaam ambapo mteja atakayeagiza vifaa vingi zaidi atapelekewa vifaa vyake popote alipo ndani ya jiji hilo bila malipo ya ziada.

’ndugu wanahabari tumekuja na progrme hii mpya na kwa sasa wateja wetu watapata punguzo kubwa la bidhaa zetu na kwa ufanisi zaidi na katika kipindi cha mwanzoni mwa usambaaji wa virusi vya corona wateja wengi walikuwa hawanunui bidhaa ila tangu rais Dkt John Magufuli alipotoa tamko kuwa watanzania waendelee kuchapa kazi hatimaye wateja wameendelea kuagiza vifaa vya ujenzi kwa wingi hivyo sisi kama FMJ tunamshukuru sana rais Magufuli kwa utendaji wake’’ alisema Bw Sanga.

Aidha ameongeza kuwa kwa sasa wameanza kufanya mnada kupitia vyombo mbali mbali vya habari ambao umerushwa mubashara na vyombo hivyo na mwitiko umekuwa mkubwa sana huku akiongeza kuwa watanzania kwa sasa wamehamasika kununua vifaa vya ujenzi vinavyotengenezwa na viwanda vya ndani jambo ambalo limechagizwa na uimarishwaji wa viwanda vya ndani chini ya usimamizi wa wizara ya viwanda na biashara.

Hata hivyo ameongeza kuwa wao kama wafanyabiashara wa vifaa vya ujenzi wataendelea kuiunga mkono serikali ya awamu ya tano kupitia jemedari wake Rais Dkt John Magufuli katika uchumi wa viwanda kwa kuhakikisha wanauza kwa wingi bidhaa zinazozalishwa na viwanda vya hapa nchini.
Kampuni hiyo ya uuzaji na usambazaji wa vifaa vya ujenzi [FMJ]ambayo iko katika eneo la buguruni kisiwani katika manispaa ya ilala jijini Dar es salaam imekuwa kampuni ya kwanza kuuza bidhaa zake za ujenzi kupitia mitandao ya kijamii na vyombo vya habari mubashara ‘LIVE’ na imeahidi kuendeleza programe hiyo na hatimaye kuifikia nchi nzima.


Hata hivyo kwa wananchi ambao wangependa kushiriki kwa   kununua bidhaa katika mnada huo wanaweza kuwasiliana na FMJ Kwa namba 0652  312438 ,0716902995  au 0717478770

Comments