SHIRIKA LA ADRA LATOA MSAADA WA VIFAA KINGA HOSPITALI YA TEMEKE,KITUO CHA AFYA TEMEKE SDA.



SHIRIKA LA ADRA LATOA MSAADA WA VIFAA KINGA  HOSPITALI YA TEMEKE,KITUO CHA AFYA TEMEKE SDA.





Dar es salaam
Shirika la maendeleo na maafa nchini Tanzania lililo chini ya kanisa la waadventista wasabato [ADRA]limetoa msaada wa vifaa kinga kwa hospitali ya rufaa ya mkoa Temeke pamoja na zahanati pamoja na kituo cha afya cha kanisa la waadventista wasabato Temeke SDA vyenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 8 kwa lengo la kuwezesha mapambano dhidi ya virusi vya Covid19 vinavyosababisha  ugonjwa wa homa kali ya mapafu Corona.

Akizungumza wakati wa makabidhiano ya vifaa hivyo yaliyofanyika jijini Dar es salaam,Askofu wa kanisa la waadventista wasabato jimbo la kusini mwa Tanzania Mark Malekana alisema kuwa vifaahivyo ambavyo ni pamoja na vitakasa mikono,barakoa na mavazi maalum ya kujikinga na virusi  vya Corona kwa wahudumu wa afya [PPE’s]ni mwendelezo wa shirika la ADRA katika kusaidia sekta ya afya hapa nchini sambamba na kuiunga mkono serikali katika mapambano juu ya Corona.
‘’tumetoa hapa leo vifaa hivi vikasaidie mapambano dhidi ya Corona ikiwa ni mwendelezo wa shirika la ADRA ambalo lilianzishwa mwaka 1973 kwa lengo la kusaidia shughuli mbali mbali katika jamii ikiwemo maji,afya na elimu hivyo tutaendelea pia katika hospitali nyingine na hatutoi msaada kwa kuangalia misingi ya kidini,kikabila au itikadi nyingine yoyote bali tunatoa kwa manufaa ya watanzania wote na pia tunamshukuru Rais Magufuli kwa kuruhusu shughuli nchini kuendelea kama kawaida kwa kuzingatia tahadhari za afya’’alisema Askofu Malekana.

Aidha Askofu Malikana amevitaka vyuo vikuu,vyuo vya elimu ya kati na shule za sekondari nchini  ambazo zinatarajiwa kufunguliwa tena june mosi mwaka huu kupanga ratiba zao za masomo kwa kuzingatia umuhimu wa ibada na Imani za watu hivyo wasiweke ratiba zinazoingilia mpaka siku za kusali na badala yake watoe fursa za kufanya ibada kwa wanafunzi katika siku za ibada kwani hata kupungua kwa maambukizi ya virusi vya corona kumesababishwa na maombi ya Watanzania hivyo shule na vyuo viheshimu ratiba ya siku za ibada.

Kwa upande wake mwakilishi wa mganga mkuu wilaya ya Temeke Dkt Grace Mtangu ambaye alipokea msaada wa vifaa kinga hivyo amelishukuru shirika la ADRA na kanisa la waadventistawasabato nchini kwa kujitoa katika katika sekta ya afya kwa kutoa misaada katika hospitali za serikali sambamba na kuendelea kutoa huduma za afya katika vituo vya afya vya kanisa hilo ambavyo  vinaisaidia serikali na jamii husika  katika sekta ya afya huku akiyataka mashirika mengine ya dini kuendelea kuiga mfano huo mzuri wa shirika la ADRA TANZANIA.
‘’hakika sisi kama hospitali ya rufaa ya mkoa,Temeke tumefurahishwa na jinsi shirika la ADRA na kanisa la waadventista wasabato lilivyojitolea kwa kutoa vifaa kinga hivi ambavyo vitaisaidia hospitali katika mapambano dhidi ya magonjwa mbalimbali ikiwemo Corona hivyo pia nawaomba wakaazi wa Temeke na watanzania kwa ujumla tendelee kuchukuatahadhari juu ya ugonjwa wa corona kwa kufuata miongozo inayotolewa na wizarayetu ya afya’’alisema Dkt Mtangu.

Naye mkurugenzi wa huduma za afya wa kanisa la waadventista wasabato jimbo la kusini,Dkt Watson Mwabase amelishukuru shirika la ADRA Kwa msaada wa vifaa kinga hivyo vilivyotolewa pia katika kituo cha afya cha kanisa cha Temeke SDA kwa kusema kuwa vitasaidia watumishi wa kituo hicho katika mapambano dhidi ya ugonjwa wa Corona.

Comments