TLP KUMUUNGA MKONO RAIS MAGUFULI KATIKA UCHAGUZI MKUU,YAUNDA KAMATI MAALUM KUMFANYIA KAMPENI


TLP  KUMUUNGA MKONO RAIS MAGUFULI KATIKA UCHAGUZI MKUU,YAUNDA KAMATI   MAALUM   KUMFANYIA KAMPENI


DAR ES SALAAM
Chama cha Tanzania Labour Party [TLP]  kimesema hakitaweka mgombea wa nafasi ya urais katika uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika baadaye mwaka huu na badala yake kitamuunga mkono rais Dkt John Magufuli kama mgombea pekee wa urais katika uchaguzi huo.
Akizungumza na wajumbe wa mkutano mkuu uliokutana hii leo jijini Dar es salaam,mwenyekiti wa chama hicho Dkt Augustino Mrema amesema kuwa chama hicho kimefikia maamuzi hayo kwa kauli moja ya kumuunga mkono Rais Magufuli kutokana na utendaji kazi wake katika kulipigania taifa la Tanzania na kuchochea kasi ya    maendeleo.
Hata hivyo Dkt Mrema amesema  kuwa chama hicho kimeshuhudia maendeleo makubwa hasa katika suala la elimu bure,ujenzi wa miundombinu ya barabara na madaraja ,kuboreshwa kwa bandari ,kufufua shirika la ndege ,kuinua sekta ya afya pamoja na kupambana na suala la ufisadi hivyo wameona hakuna anayestahili kuendelea kuwa katika nafasi hiyo isipokuwa ni Dkt John Magufuli.
‘’tumeridhika sana sisi kama TLP ,tumeangalia ilani yetu ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2015 yote ambayo tuliahidi kwa wananchi yametekelezwa na Rais Dkt John Magufuli ‘’alisema Mrema.
Naye katibu wa itikadi  na uenezi wa chama cha mapinduzi [CCM]Humphray Polepole ameipongeza hatua ya chama hicho kumteua Rais Magufuli na kumuunga mkono kama mgombea wa urais kwa mwaka 2020/2025  huku akivitaka vyama vingine vya siasa kuiga mwenendo wa chama cha TLP kwa kuachana na siasa za uchochezi  ambazo zinataka kuligawa Taifa kwa kutumika na mabeberu wasiolitakia amani taifa letu.
Kwa upande wake naibu msajili wa vyama vya siasa hapa  nchini Sisty Nyahoza amesema chama cha TLP hakijavunja katiba kumfanya Rais Magufuli kama mgombea urais na kumuunga mkono kwa asilimia 100 na kuitaja hatua ya chama hicho kama maendeleo makubwa katika mabadiliko ya kisiasa hapa nchini.
Aidha katika hatua nyingine chama hicho kimeunda kamati maalum ya kumfanyia kampeni  Rais Magufuli bega kwa bega kote nchini na kamati hiyo itatumika katika kunadi sera zake  na miradi yote ya maendeleo aliyoitekeleza

Comments