''TANZANIA NDIYO NCHI YENYE TUME HURU YA UCHAGUZI BARANI AFRIKA''MCHUNGAJI ANTHONY LUSEKELO


Mchungaji wa kanisa la Maombezi GRC jijini Dar es Salaam Anthony Lusekelo maarufu  kama  mzee wa upako amewataka vijana kujiepusha na vurugu ambazo zitahatarisha amani ya Tanzania kabla na baada ya uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika October 28 mwaka huu.

 

Rai hiyo ameitowa jijini Dar es Salaam wakati akizungumza na waandishi wa habari,ambapo amesema vijana wanatakiwa kuendeleza misingi ya amani iliyoasisiwa na mababu zao ambao ni waasisi wa Taifa.

 

Amesema kuwa kuna baadhi ya wanasiasa ambao wamekua wakiwadanganya wananchi kuwa Tume ya uchaguzi (NEC) sio huru,jambo ambalo siyo la kweli kwani barani Afrika,Tanzania pekee ndio nchi yenye Tume huru ya uchaguzi.

 

"Tume ya Taifa ya uchaguzi Tanzania ni huru ndio maana wagombea walikua na imani nayo ndio maana wakachukua fomu ya kushiriki kugombea, ila ikitokea mgombea ameshindwa ndio anaanza kusema Tume sio huru"amesema Mzee Lusekelo.

 

Hata hivyo, amesema kuwa Tanzania ni bora kuliko chama chochote Cha siasa hivyo, watanzania wanatakiwa kuepuka kutumika vibaya  katika maslahi yao binafsi.

 

Aidha, amewetaka viongozi wa dini kuacha tabia ya kuwashawishi waumini wao kuchagua mgombea wa chama fulani na badala yake waache waumini hao kufanya maamuzi ili kuepusha kuwa makundi na mganyiko katika nyumba za ibada.

Comments