TGNP MTANDAO YAADHIMISHA SIKU 16 ZA KUPINGA UKATILI WA KIJINSIA,WADAU WAPEWA NENO.

 
TGNP MTANDAO YAADHIMISHA  SIKU 16 ZA KUPINGA UKATILI WA KIJINSIA,WADAU WAPEWA NENO.



Spika Mstaafu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Anne Makinda(picha na tgnp mtandao) 


Dar es salaam

 Ikiwa ulimwengu unaadhimisha siku 16 za kupinga vitendo vya ukatili dhidi ya wanawake na watoto,kuanzia november 25 hadi desemba 10 kila mwaka,Wito umetolewa kwa wadau mbalimbali nchini  wametakiwa kutumia mpango kazi ulioandaliwa na Serikali wa kutokomeza ukatili wa kijinsia dhidi ya wanawake na watoto ili kutoa elimu  kwa jamii na kuhamasisha kutoa taarifa na kuzitunza kwa watu wanaofanyiwa vitendo vya ukatili.

 

Wito huo umetolewa jijini Dar es Salaam na Spika Mstaafu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Anne Makinda wakati alipokua katika maadhimisho ya siku 16 za kupinga  ukatili wa kijinsia yenye (muktadha miaka 25 ya Being) ambapo kauli mbiu ya maadhimisho hayo ni wekeza, wezesha tokomeza ukatili wa kijinsia.

 

Amesema kuwa, wadau mbalimbali wa kupinga vitendo vya ukatili wanapaswa kueka kumbukumbu (taarifa) za Matukio ya ukatili yanaporipotiwa ili vizazi vijavyo viweze kusoma na kujinza mambo mbalimbali ambayo yalitokea na hatua zilizochukuliwa katika kupinga vitendo vya ukatili.

 

"Nasisitiza tena naomba muzitunze taarifa zenu ambazo mnazifanya katika kutokomeza ukatili wa kijinsia zidi ya wanawake na watoto kwani Tanzania hatuna utaratibu wa kuhifadhi kumbukumbu za Matukio"amesema Makinda.

 

''Kama kauli mbiu inavyotuongoza, suala la kutokomeza ukatili wa kijinsia ni jukumu la kila mmoja katika nafasi yake. Kauli mbiu hii inatupa msukumo wa kuhakikisha kuwa kila mmoja katika nafasi yake anapaza sauti na kuchukua hatua ya kuzuia na kutokomeza vitendo vya ukatili wa kijinsia katika maeneo mbalimbali ikiwemo nyumbani, kazini, katika taasisi za elimu, katika ngazi ya jamii na serikali''amesema Makinda

Ameongeza kuwa Kutokomeza ukatili wa kijinsia ni kulinda haki za binadamu. Tunapaswa kutambua kuwa wanawake na watoto pia ni binadamu hivyo, haki zao ni haki za binadamu ambazo zinapaswa kuheshimiwa na kulindwa.  Tukumbuke kuwa tunapoangalia mustakabali wa taifa letu, ni wazi kuwa suala la kutokomeza ukatili wa kijinsia ni kipaumbele. Taifa lisilo na ukatili wa kijinsia ni taifa lenye maendeleo jumuishi, ya kasi na endelevu.

Ili kuwa na maendeleo endelevu kwa wote (Wanawake na wanaume) ni lazima kuzingatia na kuheshimu haki za binadamu. Binadamu yeyote ili aweze kushiriki kikamilifu katika shughuli za maendeleo ni lazima awe huru au asikumbane na vitendo vya ukatili.  Hivyo basi, usalama wa wanawake na watoto dhidi ya vitendo vya ukatili wa kijinsia ni jambo la msingi sana kwa maendeleo na ustawi wa taifa lolote.  

 

Naye, Mkurugenzi wa TGNP Mtandao Lilian Liundi amesema kuwa, kila mtu akisimama kwa nafasi yake kupinga ukatili wa kijinsia Tanzania itaweza kupunguza vitendo hivyo.

 

Ameongeza kuwa takwimu zinatolewa kila mwaka kuhusu hali ya ukatili nchini lakini bado hakuna   uwajibikaji wa moja kwa moja, ndio huku akitoa  mifano hai ambayo imeshatokehasa suala la kwa watoto kukatishiwa ndoto zao kwa kufanyiwa ukatili.

 

 

"Serikali yetu imejitahidi, kuweka sheria, sera na mikakati ya kutokomeza Ukatili wa Kijinsia kwa wanawake na watoto lakini changamoto ilinayofifisha jitihada hizi ni bajeti kidogo inayotengwa kuviwezesha vyombo husika. Tunaiomba serikali kuu na halmashauri zetu, zitoe kipaumbele kwenye bajeti zake katika kuwezesha dawati la Jinsia na mtoto polisi, kamati za Utekelezaji wa Mpango kazi wa Kutokomeza Ukatili kwa Wanawake na watoto (MTAKUWWA) kuanzia ngazi ya Halmashauri hadi vijiji" Lilian Liundi

Mkurugenzi wa TGNP Mtandao Lilian Liundi

 

 Kwa upande wake, Afisa Ustawi wa Jamii kutoka Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto Delius Damas amesema kuwa, Serikali inaingia garama kubwa sana katika kupambana na vitendo vya ukatili wa kijinsia.

 

Amesema kuwa, Serikali imeandaa mpango kazi wa kupinga ukatili wa kijinsia dhidi ya wanawake na watoto kwa lengo la kupunguza vitendo hivyo kwa asilimia 50 kabla ya 2022.

 

"Tumejipanga kuweka madawati ya kijinsia shule zote ili wanafunzi waweze kutoa taarifa za vitendo vya ukatili wanapofanyiwa ikiwemo shuleni, majumbani na sehem nyengine"amesema Damas.



 

 


Comments