VIONGOZI WA DINI WAWATAKA WATANZANIA KUENDELEA KUDUMISHA AMANI

VIONGOZI WA DINI WAWATAKA WATANZANIA KUENDELEA KUDUMISHA AMANI




Dar es salaam.

Watanzania wamewataka kuendelea kudumisha amani na utulivu nchini ili kuwa na misingi bora katika uboreshaji wa maendeleo.
Hayo yamesemwa na Mwenyekiti wa Kamati ya Dini mbalimbali (ISCEJIC) Askofu Stephen Munga Katika kongamano la viongozi wa Dini pamoja wadau wa usalama nchini ambalo limefanyika kwa lengo la kujadili nafasi ya viongozi wa dini katika kudumisha Maendeleo nchini linalofanyika kwa siku mbili katika ukumbi wa baraza kuu la maaskofu katoliki TEC,Kurasini jijini Dar es salaam.


Askofu Munga amesema suala la maendeleo kwa katika nchi ambayo haina amani itakuwa ni miujiza hivyo ni vyema wananchi pamoja na viongozi kwa ujumla wakaendelea kuitunza amani ya nchi yetu.

Naye katibu mkuu wa baraza la maaskofu Tanzania TEC,Padri Charles Kitima amesema viongozi wanapaswa kuwaheshimu wananchi wanaowaongoza kwani wao ndiyo wamewaweka katika madaraka hivyo wanafaa kuwatumikia bila ubaguzi wowote huku akiongeeza kuwa kongamano hilo litakuwa ni chachu ya maendeleo ya Taifa katika kukuza demokrasia na kuendeleza amani ya Taifa.

Aidha Padri Kitima ameongeza kuwa ni muhimu kwa viongozi wa serikali,kisiasa,kidini na wananchi wakawa na mahusiano mazuri ambayo yatachochea maendeleo ambayo hayatajali itikadi zao jambo ambalo litaendelea kuitunza amani ya Tanzania na kuchochea maendeleo.


Naye mjumbe wa baraza la ulamaa [Bakwata Taifa]Sheikh Issa Mohammed Issa amesema kuwa kongamano hilo la viongozi wa dini mbali mbali linapaswa kuja na mapendekezo yatakalolijenga taifa letu kwa umoja na amani kwani viongozi wa dini wana nafasi kubwa katika kuendeleza amani kupitia mafundisho yao katika nyumba za ibada.


Kwa upande wake mkuu wa polisi Mkoa wa Temeke, Amon Kakwale akizungumza kwa niaba ya IGP Simon Sirro katika mkutano uliowakutanisha viongozi wa dini kujadili amani na maendeleo baada ya uchaguzi mkuu wa mwaka huu.amesema viongozi wa dini wanafanya kazi kubwa ya kuhubiri amani jambo linalowarahisishia kazi polisi katika utekelezaji wa majukumu yao.

“Sisi ni makamanda wa kimwili na kiakili, kazi yetu ni kuwakamata na kuwapeleka kwenye vyombo vya sheria wanaovunja amani kwa namna yeyote ile. Ninyi wenzetu ni makamanda wa kiroho, mnafanya doria za kiroho kusaidia kuwafanya watu kuwa na hofu ya Mungu na kutambua umuhimu wa kulinda na kuitunza amani,” amesema Kakwale.

Kamanda huyo ameongeza kuwa ipo migogoro mingi ambayo viongozi wa dini wanatumia nyumba za Ibada kuitatua kwa lengo la kunusuru nchi kuingia kwenye machafuko.

Kwa upande wake, Askofu Jacob Chimeledya amesema ipo haja kwa viongozi wa dini kukutana na wa vyama vya siasa kujadili mustakabali wa amani ya Taifa hili.

Comments