[NEEC]YAWATAKA WANANCHI KUCHANGAMKIA FURSA KATIKA MAONYESHO YA 4 YA MIFUKO NA PROGRAME ZA UWEZESHAJI

 [NEEC] YAWATAKA WANANCHI KUCHANGAMKIA FURSA KATIKA MAONYESHO YA 4 YA MIFUKO NA PROGRAME ZA UWEZESHAJI.


DAR ES SALAAM.

Wananchi wa jiji la Arusha na mikoa ya jirani wametakiwa kujitokeza kwa wingi na kuchangamkia fursa katika maonyesho ya nne ya mifuko  na program za uwezeshaji wananchi kiuchumi yatakayofanyika jijini humo mwezi february 2021.

Akitoa taarifa mbele ya wabahabari jijini Dar es salaam katibu mtendaji wa baraza la Taifa la  uwezeshaji wananchi kiuchumi [NEEC] Bi Beng'i Issa  amesema kuwa maonyesho hayo yana dhumuni la kukuza uelewa kwa wananchi kuhusu uwepo,majukumu na vigezo vinavyotumiwa katika kutoa huduma za mifuko ya uwezeshaji ili kuhamasisha wananchi kunufaika na fursa zilizopo katika mifuko hiyo pamoja na kutoa elimu kwa wananchi juu ya kujenga utamaduni wa kuweka akiba.

Aidha katibu huyo mtendaji wa [NEEC] ameongeza kuwa watanzania wanapaswa kuwa na utaratibu mzuri wa kuweka akiba na kuwekeza katika miradi yenye kuleta faida kupitia uanzishwaji na uimarishwaji wa vikundi vya kifedha vya kijamii ikiwemo Vikoba.

Hata hivyo ameendelea kuwa katika maonyesho hayo taasisi za umma,binafsi ,vikundi vya kifedha,mashirika ya kimataifa na asasi za kiraia zitashiriki kikamilifu maonyesho hayo yaliyoandaliwa na baraza la Taifa la  uwezeshaji wananchi kiuchumi [NEEC] ambapo yatahusisha mikoa yote ya kanda ya kaskazini ikiwemo,Kilimanjaro,Tanga,Manyara na Arusha.

 

Maonyesho hayo yatafanyika katika viwanja vya sheikh  Amri Abeid [Stadim] katika jiji la  Arusha kuanzia february 7 hadi 13 mwaka huu ambapo mgeni rasmi katika maonyesho hayo anatarajiwa kuwa waziri mkuu wa jamhuri ya muungano wa Tanzania MH. KASIM MAJALIWA

Comments