MSHINDI MISS TANZANIA EASTERN ZONE KUZAWADIWA KITITA.

 MSHINDI MISS TANZANIA EASTERN ZONE KUZAWADIWA KITITA.


Dar es salaam.

Lile shindano lililokuwa likisubiriwa kwa hamu na mashabiki wa tasnia ya urembo kanda ya Mashariki lijulikanalo kama Miss Tanzania Eastern  Zone linatarajiwa lifanyika septemba 24  mkoani Morogoro.

 

Akitoa taarifa ya fainali za shindano hilo  mbele ya wanahabari jijini Dar es salaam,Mkurugenzi wa kampuni ya Tips Forum Mhandisi Nancy Matta ambao ndiyo waandaaji na waratibu wa shindano hilo amesema maandalizi yake yamekamilika kwa kiasi kikubwa ambapo mshindi wa mashindano hayo atawakilisha katika mashindano ya kitaifa ya Miss Tanzania.

Amesema kuwa mashindano hayo yalianza ngazi za mikoa katika mikoa ya Lindi,Mtwara,Pwani na Morogoro na kupatikana washindi 16 ambao watashiriki katika fainali ngazi ya kanda ya Mashariki.

Ameongeza kuwa mashindano hayo yanatarajiwa kufanyika katika hoteli ya Morena mkoani humo ambapo mshindi wa kwanza atapata kitita cha shilingi milioni 2,mshindi wa pili sh milioni 1.5  na mshindi wa tatu atajinyakulia kitita cha sh milioni 1.

Aidha amesema kuwa lengo la kuanzisha mashindano hayo ni kukuza sekta ya urembo hapa nchini na kuutangaza utalii ndani na nje ya nchi kupitia mashindano hayo.

Nao baadhi ya wadhamini wa mashindano wakiwemo bodi ya Taifa ya utaliii TTB ambayo imewakilishwa na BI Maria Mafie ambaye amesema bodi hiyo imeamua kudhamini mashindano hayo ili kuendelea kukuza sekta ya utalii ndani na nje ya nchi kupitia mashindano ya ulimbwende.

Kwa upande wake Meneja mauzo wa hoteli ya Serena Shaban  Kaluse amesema mashindano hayo yatakuwa chachu ya kuutangaza utalii wa Tanzania.

Naye Niwako Charles ambaye ni afisa masoko hoteli ya Dynasty Beach ambapo washiriki wa kinyanganyiro hicho wameweka kambi katika hoteli hiyo amesema kuwa wataendelea kuunga mkono mashindano hayo ambayo yatatoa mlimbwende atakayeiwakilisha kanda ya kati katika mashindano ya Miss Tanzania.

Mashindano hayo yamedhaminiwa na makampuni mbali mbali ambapo mdhamini mkuu ni chanel ya utalii ya  Taifa kupitia shirika la utangazaji Tanzania ,[Tanzania Safari Channel].

Comments