TRC YASAINI MKATABA NA KAMPUNI YA CRRC INTERNATIONAL KUTENGENEZA MABEHEWA YA SGR
TRC YASAINI MKATABA NA KAMPUNI YA CRRC INTERNATIONAL KUTENGENEZA MABEHEWA YA SGR
Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Makame Mbarawa ameiagiza Bodi ya Wakurugezi ya Shirika la Reli Nchini (TRC) kuhakikisha inasimamia kwa uzalendo utengenezaji wa Mabehewa ya Treni iyendayo kwa kasi (SGR) ambayo yatatengenezwa na Kampuni kutoka China inayofahamika kama CRRC inaternational. Waziri Mbarawa ametoa maagizo hayo Jijini Dar es Salaam wakati wa kutiliana saini mkataba wa mwaka mmoja wa utengenezaji wa mabehewa yapatayao 1430 yatakayogharimu dola za kimarekani milioni 127.2 sawa na fedha za kitanzani kiasi cha zaidi ya shilingi bilioni 300. Aidha amesema kwamba utengenezaji wa mabehewa hayo unapaswa kukamilika katika muda uliopangwa kwa mujibu wa Mkataba ,nakwamba Bodi ya Wakurugenzi pamoja na timu itakayoenda nchini China kukagua utengenezaji huo inapaswa kuhakikisha mabehewa hayo yanakua na ubora unaotakiwa. " Huu mradi unatakiwa ukamilike kwa muda uliopangwa naomba nitoe maagizo kwenu Bodi ya Wakurugenzi wa TRC na timu ya watu mtakaoenda china kuangalia utengenezaji wa mabehewa haya kuhakikisha mnafanya kazi hiyo kwa uzalendo,mabehewa yawe na kiwango cha ubora unaotakiwa,pia msikubali eksichuzi zozote tunataka mradi huu ukamilike kwa haraka ili ujenzi wa reli unapokamilika mabehewa yawe tayari"amesema Waziri Mbarawa. Nae Meneja Mkuu Msaidizi wa Kampuni ya CRRC International Tang Yun Peng ameihakikishia TRC kufanya kazi hiyo kwa kuzingatia makubaliano yakimkataba yaliyosainiwa huku akiipongeza Tanzania kwamba endapo mradi wa SGR utakamilika utafungua milango yakiuchumi kwa nchi zingine za africa Mashariki.
|



Comments