CUF YATANGAZA MAAZIMIO YA BARAZA KUU LA CHAMA,YAMTEUA  HAMAD MASOUD HAMAD KUWA KATIBU MKUU.

Dar es salaa,Tanzania


Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi CUF Prof Ibrahim Lipumba amesema baraza kuu la chama hicho limemteua Ndugu Hamad Masoud Hamad kuwa katibu mkuu wa chama hicho.

Profesa Lipumba ameyasema hayo mara baada ya kuzungumza na wanahabari ofisi ya makao makuu ya chama hicho,Buguruni Jijini Dae es salaam alipokuwa akizungumzia maazimio mbalimbali ya kikao cha baraza kuu la uongozi la chama hicho lililokutana march 24 na 25 jijini humo.

Aidha mwenyekiti huyo amewapongeza wanachama wa chama hicho waliorejea katika chama mara baada ya kuondoka katika vyama walivyohamia kwa  kile walichodai haki inapatikana ndani ya chama hicho na kuongeza kwa kipindi hiki wamewaruhusu wanachama hao kugombea nafasi za uongozi ndani ya chama katika uchaguzi utakaofanyika may 14 mwaka huu katika jumuiya zote za chama hicho.

Katika hatua nyingine ameiomba serikali kuangalia namna ya kupambana na tatizo la mfumuko wa bei kwani linawaumiza wananchi wengi na kuwasababishia maisha magumu huku akitoa wito kwa Urusi na Ukraine ambao ni wazalishaji wakubwa wa ngano na mafuta ya alizeti kuketi meza moja ili kuzungumnza na kufikia muafaka wa kusitisha mapigano yanayoondoa mamia ya wananchi wasio na hatia na kuongeza kuwa chama hicho hakipendezwi na hatua ya Urusi kuivamia na kuishambulia nchi ya Ukraine.

Kuhusu suala la katiba mpya na tume huru ya uchaguzi Prof Lipumba amesema suala hilo ni muhimu na chama chake hakijapendezwa na maoni ya kikosi kazi kiluichodai suala hilo lishughulikiwe mwaka 2025 baada ya uchaguzi.

Comments