NAIBU WAZIRI DKT. KIRUSWA KUSHIRIKI MKUTANO WA UWEKEZAJI RASILIMALI ZA MADINI, NISHATI NIGERIA

 

NAIBU WAZIRI DKT. KIRUSWA KUSHIRIKI MKUTANO WA UWEKEZAJI RASILIMALI ZA MADINI, NISHATI NIGERIA




Naibu Waziri wa Madini Dkt. Steven Kiruswa  na Watalaam  kutoka Wizarani wanatarajia kushiriki  Mkutano wa Uwekezaji katika Rasilimali za Madini na Nishati utakaofanyika kuanzia tarehe 31 Mei hadi 3 Juni, 2022 nchini Nigeria.

Leo Mei 30, Naibu Waziri Dkt.Kiruswa amekutana na Balozi wa Tanzania nchini Nigeria Mhe. Benson Bana ambaye amemweleza kuhusu nia ya Mfanyabiashara  mkubwa wa nchini humo Aliko Dangote kuwekeza   katika kiwanda kikubwa cha mbolea nchini.


Comments