Skip to main content

CCM YAKUBALI UPATIKANAJI KATIBA MPYA

 

CCM YAKUBALI UPATIKANAJI KATIBA MPYA

Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Rais Samia Suluhu Hassan akiendesha Kikao Cha Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya CCM, kilichofanyika katika Ukumbi wa Jengo la Makao Makuu ya CCM la White House Jijini Dodoma, leo. Kushoto ni Makamu Mwenyekiti wa CCM Bara Kanali Mstaafu Abdulrahman Kinana.
Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa,itikadi na Uenezi (NEC)Shaka Hamdu Shaka akizungumza na waandishi wa habari leo

Na Dotto Kwilasa, Malunde 1 blog DODOMA

MWENYEKITI wa Chama cha Mapinduzi (CCM) ambae pia ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan, ameongoza Kikao cha Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi (CCM) iliyokutana leo Juni 22, 2022 katika Ukumbi wa (White House) Makao Mkuu ya CCM Jijini Dodoma ikiwa ni utaratibu wa vikao vyake vya Kitaifa.


Hatua hii imekuja baada ya Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) kukutana jana tarehe 21/06/2022 Ikulu Chamwino, Dodoma kwa kikao cha siku moja cha kawaida na kufuatia kikao cha Halmashauri Kuu ya Taifa kilichofanya uchaguzi wa kujaza nafasi mbili za wajumbe wa Kamati Kuu ya Halmashauri ya Taifa zilizokuwa wazi kwa kuwachagua kwa kura Stephen Masatu Wassira na Ndugu Theresia Adriano Mtewele.

Comments