NSSF YAFADHILI SH M. 500 UTENGENEZWAJI WA KAZIDATA YA DIASPORA

 

NSSF YAFADHILI SH M. 500 UTENGENEZWAJI WA KAZIDATA YA DIASPORA

Mwakilishi wa Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi James Bwana (wa pili kulia) na Mwakilishi wa Mkurugenzi Mkuu wa NSSF Bw. Ibrahim Maftah (wa pili kushoto) wakiwa na wanasheria wao wakisaini  makubaliano ya kuipatia Wizara Shilingi Milioni 50 kwa ajili ya kufadhili  utengenezaji wa Mfumo wa Kidigitali wa kutunza taarifa za Diaspora, (Diaspora Digital Hub) iliyofanyika katika Ofisi ndogo za Wizara jijini Dar Es Salaam.
Mwakilishi wa Mkurugenzi Mkuu wa NSSF Bw. Ibrahim Maftah akizungumza baada ya hafla ya utiaji, saini  makubaliano ya kuipatia Wizara Shilingi Milioni 50 kwa ajili ya kufadhili utengenezaji wa Mfumo wa Kidigitali wa kutunza taarifa za Diaspora, (Diaspora Digital Hub) iliyofanyika katika Ofisi ndogo za Wizara jijini Dar Es Salaam, aliyekaa kushoto ni Mkurugenzi wa Diaspora Wizarani Balozi James Bwana akimsikiliza

Na PrayGod Thadei

Katika  kuunga  mkono   juhudi  za  Serikali  ya  Awamu  akimsikiliza

 zinazongozwa  na  Rais  Samia  Suluhu  Hassan katika  kuhakikisha  Diaspora  wanachangia   kikamilifu  na  kuwa sehemu  muhimu   katika  maendeleo  ya  uchumi  wa  taifa  Mfuko  wa  Taifa  wa  Hifadhi  ya  jamii  NSSF  Umeweka wazi  kuwa  Diaspora  ni  kundi  muhimu  katika  uwekezaji  nchini.

Hayo   yameelezwa   leo Agosti 26,2022   jijini  Dar  es Salaam  na  Mkurugenzi  wa  Uthaminishaji , Takwimu  na  Usimamizi  wa  habari  na mwakilishi  wa  Mkurugenzi  mkuu  wa  NSSF  Ibrahim  Zakaria  Maftah  wakati  wa  hafla  fupi  ya  utiaji  saini  hati  ya  Makubaliano  ya  wizara  ya  mambo  ya  nje  na ushirikiano  wa  Afrika  Mashariki  na  NSSF  kwa  ajili  ya  kupokea  ufadhili  wao  katika  matengenezo  ya  Mfumo  wa  kutunza  taarifa  za  Diaspora  Kidigitali .

Ibrahim   Maftah   amesema  mfumo  huo  utatoa  uratibu   wa  kazi mbalimbali  za Diaspora kufanyika  kwa  mtandao  kitendo   kitakachopelekea  kutoa   fursa   kwa   NSSF  kutangaza  fursa  za  miradi  mbalimbali   ya   uwekezaji   zitolewazo  na   mfuko 

“Kitendo cha NSSF kusaini makubaliano hayo kinaonesha utayari na muelekeo wetu katika kutumia fursa mbalimbali zinazopatikana katika eneo la Diaspora,” alisema Bw. Maftah.

Kwa  upande  wake  mkurugenzi  wa  Kitengo  cha  Diaspora  na  mwakilishi  wa  Katibu  Mkuu  wa  Wizara  ya  Mambo  ya  Nje  na  Ushirikiano  wa  Afrika  Mashariki  Balozi  James  Bwana  amesema   kupitia  makubaliano  walioingia   na  NSSF wanaimani 

kuwa   kupitia   mfumo    huo  kutawezesha   kuwasajili   na  kuwatambua   Diaspora  Watanzania   waliopo   katika  mataifa  mbalimbali   ulimwenguni  na  kuwawezsha  kupata   huduma  za  kimaendeleo , biashara , uchumi  na  uwekezaji  hapa  nchini .

“Leo hii tumeshuhudia utiaji saini wa makubaliano ambayo yataiwezesha NSSF kutoa Shilingi Milioni 50 ambazo zitaiwezesha Wizara kutengeneza Mfumo wa Kidigitali wa kutunza taarifa za Diaspora, kitendo hiki ni mwanzo wa ushirikiano wa muda mrefu ambao Wizara umekuwa nao na NSSF, ni matarajio ya Wizara kuwa NSSF itahuisha program yao ya Diaspora na kubuni programu mpya ili kutoa huduma kwa Diaspora wetu na wao kunufaika zaidi na programu hizo,” alisema Balozi Bwana.


Comments