Skip to main content

MKUTANO WA WADAU VYUO VYA UTALII WAFUNGULIWA DAR,WAZIRI AWASHAURI WAWEKEZAJI KUWEKEZA MIKOA YA KUSINI

 

MKUTANO WA WADAU VYUO VYA UTALII WAFUNGULIWA DAR,WAZIRI AWASHAURI WAWEKEZAJI KUWEKEZA MIKOA YA KUSINI

Waziri wa maliasiali na utalii,Balozi Dkt Pindi Chana akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani)

Waziri wa Mali Asili na Utalii Balozi Dkt  Pindi Chana amewashauri wawekezaji wanaotaka kuwekeza katika sekta ya utalii hapa nchini kuwekeza katika mikoa ya Kusini kwa mwa Tanzania. 

Dkt.Pindi Chana ameyasema hayo alipokuwa akifungua mkutano wa siku mbili uliowakutanisha wadau kutoka vyuo mbalimbali vya utalii nchini na serikali kujadili namna ya kuendeleza sekta ya utalii licha ya uwepo wa janga la Corona unaofanyika katika ukumbi wa mikutano wa kimataifa wa mwalimu Nyerere jijini Dar es salaam ulioandaliwa na chuo cha Taifa cha utalii.

 Aidha amesema kubwa kwa sasa sekta ya utalii ni soko kubwa ambalo kuzalisha ajira na kuongeza pato la taifa hivyo jitihada mbalimbali zinaendelea kufanyika kuboresha Sekta hiyo.

Amesema kuwa serikali kupitia chuo cha Taifa cha utalii imekuwa ikitoa elimu bora kwa watumishi na wahudumu wa hoteli za kitalii na kuchangia katika uboreshaji wa sekta ya utalii kwa kuwafundisha ukarimu wahitimu wa chuo hicho pindi waingiapo makazini.

Kuhusu mpango wa wizara ya maliasili na utalii wa kukuza utalii katika mikoa ya Kusini Balozi Dkt Pindi Chana amewashauri wawekezaji wa hoteli kuwekeza katika hifadhi za taifa zilizopo katika mikoa ya kusini nwa Tanzania katika Masuala ya hoteli na sehemu za kulala wageni ndani ya hifadhi hizo ili kuweza kuboresha Sekta hiyo.

Advertisements
REPORT THIS AD” Maeneo ya Uwekezaji wa Hoteli na sehemu zakulalawageni bado ni hitaji kubwa katika utalii wa kusini mwa Tanzania hivyo wawekezaji wachangamkie fursa hiyo” Amesema Balozi Chana.Hata hivyo amesema kumekuwa na mwitikio mkubwa kwa watalii kutokana na filamu Royal Tour idadi kubwa ya watalii wamekuwa wakija nchini Tanzania hivyo nifursa kwa wafanyabishara wa sekta ya utalii kukuza Biashara zao kupitia Sekta hiyo.

Kwa upande wake Kaim Afisa Mkuu wa Chuo cha Utalii Dkt. Florian Mtei amesema katika mkutano huo watapitia tafiti zilizofanywa na wataalamu kutokana nchi mbalimbali ikiwemo Afrika Kusini kuangalia changamoto zilizosababishwa na janga la Covid 19 na jinsi ya kukabiliana nazo ili kukuza sekta ya utalii.

Dkt Mtei amesema kuwa dhamira ya chuo cha TAIFA cha utalii kuandaa mkutano huo ni ili kuunga mkono juhudi za serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na rais Samia Suluhu Hassan ambaye ana dhamira ya dhati ya kuuza sekta ya utalii hapa nchini na duniani,pamoja na kukutana na wadau kujadili masuala mbalimbali ya utalii.

Sambamba na hayo amesema kuwa kupitia mkutano huo wataweza kuweka mikakati kama nchi kuangalia njia gani wanazoweza kufanya kuepukana na majanga kama Covid 19 yanayoisumbua Duniani.

Comments