TMA YATANGAZA UWEPO WA MVUA ZA EL-NINO,YATOA TAHADHARI HII

 


Hali ya joto la Bahari katika eneo la kati la kitropiki la bahari ya Pasifiki linatarajiwa

kuendelea kuwa la juu ya wastani katika kipindi cha Novemba, 2023 hadi Aprili, 2024. Hali

hii inaashiria kuendelea kuwepo kwa hali ya El-Niño. Hata hivyo, hali ya El-Niño inatarajiwa

kupungua nguvu kadiri tunavyoelekea mwisho wa msimu wa mvua. Kwa upande wa Bahari

ya Hindi, hali ya joto la bahari la juu ya wastani inatarajiwa kuendelea kuwepo upande wa

magharibi mwa bahari kwa msimu wote wa mvua za Novemba, 2023 hadi Aprili, 2024. Hali

kadhalika joto la bahari la chini ya wastani hadi wastani linatarajiwa kuendelea kuwepo kwa

upande wa mashariki mwa Bahari ya Hindi, hususan katika kipindi cha nusu ya kwanza ya

msimu. Hali hii inaashiria kuendelea kuwepo kwa hali inayotambulika kama “Positive Indian

Ocean Dipole (IOD)” katika nusu ya kwanza ya msimu wa mvua na baadae kupungua

nguvu katika nusu ya pili ya msimu (Februari hadi Aprili, 2024). Kwa upande wa Bahari ya

Atlantiki, joto la bahari la wastani hadi Juu kidogo ya wastani linatarajiwa kuwepo katika

eneo la mashariki mwa bahari.

Kwa ujumla hali hii inatarajiwa kuimarisha mifumo inayosababisha mvua nchini hasa kipindi

cha nusu ya kwanza ya msimu.

Kwa upande mwingine, upepo kutoka misitu ya Kongo kuelekea nchini unatarajiwa

kuimarika hasa katika nusu ya kwanza ya msimu. Hali hii inatarajiwa kuimarisha makutano

ya upepo katika maeneo ya kati na mashariki mwa nchi, hali itakayochangia kuimarisha

mifumo isababishayo mvua nchini.

3. ATHARI NA USHAURI

Athari na ushauri umeandaliwa na Mamlaka ya Hali ya Hewa kwa kushirikiana na wataalam

wa sekta husika katika mkutano wa wadau wa hali ya hewa uliofanyika tarehe 27

Oktoba, 2023.

a) Kilimo na Usalama wa Chakula

Vipindi vya unyevu wa kuzidi kiasi pamoja na mafuriko vinaweza kujitokeza na kuathiri

ukuaji wa mazao na miundombinu ya kilimo. Magonjwa kama vile ukungu (Fungus)

yanatajariwa kuongezeka na kuathiri mazao kama viazi mviringo, nyanya, ufuta na

maharage. Hata hivyo, shughuli za kilimo zinatarajiwa kuendelea kama ilivyo kawaida

hususan katika maeneo yanayotarajiwa kupata mvua za Wastani hadi Juu ya Wastani

Wakulima wanashauriwa kuandaa mashamba, kupanda, kupalilia na kutumia pembejeo

husika kwa wakati, kutumia mbinu bora na teknolojia za kuzuia maji kutuama shambani,

mmomonyoko na upotevu wa rutuba, na kuchagua mbegu na mazao sahihi kwa ajili ya

msimu huu. Aidha, inashauriwa kuimarisha miundombinu ya kilimo pamoja na uvunaji

maji ya mvua na kudhibiti visumbufu vya mimea ili kupunguza athari zinazoweza

kujitokeza.


b) Mifugo na Uvuvi

Wafugaji na wavuvi wanatarajiwa kufaidika na upatikanaji wa malisho, maji na chakula

cha samaki. Hata hivyo, milipuko ya magonjwa ya mifugo kama vile ugonjwa wa homa ya


Mawasiliano yote yaelekezwe kwa:


Mkurugenzi Mkuu, Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania, Chuo Kikuu cha Dodoma,

Jengo la Utawala, Ndaki ya Sayansi za Kompyuta na Elimu Angavu, 1 Mtaa wa CIVE,

S.L.P 27, 41218 Dodoma; Simu: +255 26 2962610: Nukushi: +255 26 2962610

Barua pepe; met@meteo.go.tz; Tovuti: www.meteo.go.tz


(IMETHIBITISHWA – ISO 9001:2015, Huduma za Hali ya Hewa kwa Usafiri wa Anga)


Page 6 of 10 727K – 03/2023

bonde la ufa, midomo na kwato, na kuzaliana kwa wadudu wanaosambaza magojwa

inaweza kujitokeza. Vilevile, matukio ya kuongezeka kwa magonjwa ya mwani baharini na

kupungua kwa uzalishaji wa mwani kutokana na kupungua kwa kiwango cha chumvi ya

maji ya bahari vinatarajiwa. Aidha, uharibifu wa mabwawa ya samaki kutokana na

ongezeko la mvua unaweza kujitokeza.

Wafugaji wanashauriwa kutumia mbinu bora za ufugaji ili kutunza malisho na kuvuna maji

ya mvua kwa matumizi ya baadae. Jamii inashauriwa kuweka mipango mizuri ya

matumizi bora ya maji na malisho. Wakulima wa mwani wanashauriwa kulima mwani

kwenye maji ya kina kirefu ili kuondokana na athari za maji ya mvua yanayokuwa

yanaingia baharini. Aidha, Wafugaji na wavuvi wanashauriwa kufuatilia mirejeo ya tabiri

za hali ya hewa na ushauri kutoka kwa maafisa ugani ili kupunguza athari zinazoweza

kujitokeza na kuongeza tija katika msimu huu wa mvua.

c) Utalii na Wanyamapori

Hali ya malisho na maji kwa ajili ya wanyamapori katika mbuga na hifadhi inatarajiwa

kuwa nzuri. Hata hivyo, wingi wa mvua unaotarajiwa katika maeneo mengi unaweza

kusababisha kutuama na kusambaa kwa maji na kupelekea wanyamapori kuhama,

hususan katika maeneo yanayotarajiwa kupata mvua za Juu ya Wastani hadi Wastani.

Hali hii inaweza kusababisha magonjwa ya wanyamapori kusambaa kwa wanyama

wanaofugwa na binadamu kutokana na wanyamapori kuingia katika makazi ya jamii

zinazozunguka hifadhi na mbuga. Pia, hali hii inaweza kusababisha hatari kwa binadamu

na wanyama wanaofugwa kutokana na kushambuliwa na wanyama wakali.

Mamlaka husika zinashauriwa kuboresha miundombinu mbalimbali katika hifadhi za

wanyamapori na kujenga uelewa kwa jamii ili kupunguza athari zinazoweza kujitokeza

kutokana na hali ya mvua inayotarajiwa. Hivyo basi, jamii inashauriwa kutoa taarifa kwa

mamlaka husika iwapo wanyamapori wataingia katika makazi au maeneo mbalimbali ya

watu.

d) Usafiri na Usafirishaji

Kutokana na utabiri huu, miundombinu ya usafiri na usafirishaji inaweza kuathirika

hususan maeneo yanayotarajiwa kupata mvua za Juu ya Wastani. Matukio ya hali mbaya

ya hewa yanaweza kuharibu miundombinu ya barabara na reli, ongezeko la ajali

barabarani katika usafiri wa nchi kavu (barabara na reli); kuchelewa au kusitishwa kwa

safari za ndege na reli; mawasiliano hafifu angani na majini; na kuongezeka kwa gharama

za uendeshaji katika shughuli za usafiri na usafirishaji kwa ujumla. Wadau wa sekta hii

wanashauriwa kuchukua hatua stahiki katika utekelezaji wa ujenzi wa miundombinu

mbalimbali pamoja na ukaguzi wa mara kwa mara wa miundombinu ya usafiri na

usafirishaji ili kupunguza athari zinazoweza kujitokeza.

e) Nishati, Maji na Madini

Upatikanaji wa maji unatarajiwa kuimarika, hususan katika maeneo yanayotarajiwa kupata

mvua za Wastani na Juu ya Wastani. Kina cha maji katika mabwawa, maziwa na mito

kinatarajiwa kuongezeka. Hivyo, athari katika miundombinu ya rasilimali maji, usambazaji


Mawasiliano yote yaelekezwe kwa:


Mkurugenzi Mkuu, Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania, Chuo Kikuu cha Dodoma,

Jengo la Utawala, Ndaki ya Sayansi za Kompyuta na Elimu Angavu, 1 Mtaa wa CIVE,

S.L.P 27, 41218 Dodoma; Simu: +255 26 2962610: Nukushi: +255 26 2962610

Barua pepe; met@meteo.go.tz; Tovuti: www.meteo.go.tz


(IMETHIBITISHWA – ISO 9001:2015, Huduma za Hali ya Hewa kwa Usafiri wa Anga)


Page 7 of 10 727K – 03/2023

maji, uchimbaji mdogo wa madini na nishati inaweza kujitokeza. Shughuli za uchimbaji

madini hususan katika migodi midogo zifanyike kwa kuzingatia tahadhari zinazotolewa

kwani ongezeko la maji katika udongo linaweza kusababisha maporomoko ya ardhi.

Wadau wanashauriwa kuzingatia matumizi endelevu na uhifadhi wa rasilimali maji katika

shughuli za uchakataji wa madini, uzalishaji wa umeme, matumizi ya viwandani na

majumbani. Hali kadhalika, mamlaka husika zinashauriwa kuimarisha miundombinu ya

rasimali za maji na kuweka mipango madhubuti ya uzalishaji wa nishati ya umeme kutoka

vyanzo mbadala kama vile nishati ya jua, jotoardhi, upepo na gesi endapo kutatokea

uharibifu wa miundombinu kutokana na athari za mvua za Juu ya Wastani.

f) Mamlaka za Miji na Wilaya

Vipindi vya mvua kubwa vinaweza kusababisha kutuama kwa maji na mafuriko. Hali hii

inaweza kusababisha uharibifu wa miundombinu na upotevu wa maisha na mali. Mamlaka

za Miji na Wilaya zinashauriwa kuboresha mifumo ya mifereji ya maji ili kupunguza athari

zinazoweza kusababishwa na mafuriko sambamba na kutoa elimu kwa jamii juu ya hatua

zinazopaswa kuchukuliwa. Hatua hizo ni pamoja na kuimarisha Kamati za Usimamizi wa

Maafa ngazi za kijiji na Wilaya ili ziweze kujiandaa, kukabiliana na kupunguza athari pindi

zitakapotokea.

g) Sekta ya Afya

Magonjwa ya mlipuko yanaweza kujitokeza kutokana na uharibifu wa miundombinu ya maji

taka unaoweza kusababishwa na maji kutuama na kutiririka. Hivyo, jamii inashauriwa

kuchukua hatua kuhakikisha usafi wa mazingira yanayowazunguka, kuharibu mazalia ya

mbu na kudumisha usafi kwa ujumla. Mamlaka za afya zinashauriwa kuchukua hatua

stahiki kupunguza athari zinazoweza kujitokeza, ikiwa ni pamoja na kuhimiza wananchi

kutibu maji kabla ya kutumia, pamoja na kunywa maji safi na salama. Pia, kuhakikisha

uwepo wa dawa za kutosha katika vituo vya afya kwa kuzingatia uwezekano wa uharibifu

wa miundombinu ya usafirishaji.

h) Sekta Binafsi

Shughuli za kilimo na uzalishaji viwandani zinatarajiwa kunufaika kutokana na mvua za

kutosha zinazotarajiwa katika msimu huu. Hata hivyo, wingi wa mvua unaweza kupelekea

athari katika shughuli za ujenzi wa miundombinu, uhifadhi na usafirishaji wa mazao tete

na bidhaa.

Wadau wa Sekta Binafsi wanashauriwa kushirikiana na wataalamu mbalimbali ikiwemo

wataalam wa hali ya hewa ili kukabiliana na athari zinazoweza kujitokeza. Taasisi za

Benki na Bima zinashauriwa kuandaa na kutoa huduma mahususi kwa wadau ili kujenga

ustahimilivu katika biashara.

i) Menejimenti za Maafa


Mawasiliano yote yaelekezwe kwa:


Mkurugenzi Mkuu, Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania, Chuo Kikuu cha Dodoma,

Jengo la Utawala, Ndaki ya Sayansi za Kompyuta na Elimu Angavu, 1 Mtaa wa CIVE,

S.L.P 27, 41218 Dodoma; Simu: +255 26 2962610: Nukushi: +255 26 2962610

Barua pepe; met@meteo.go.tz; Tovuti: www.meteo.go.tz


(IMETHIBITISHWA – ISO 9001:2015, Huduma za Hali ya Hewa kwa Usafiri wa Anga)


Page 8 of 10 727K – 03/2023

Katika maeneo yanayotarajiwa kupata mvua za Juu ya Wastani hadi Wastani vipindi vya

mvua kubwa vinaweza kujitokeza na kusababisha mafuriko na maporomoko ya ardhi na

kupelekea uharibifu wa miundombinu, mazingira, upotevu wa mali na madhara kwa

binadamu. Hivyo, Idara ya Menejimenti ya Maafa nchini inashauriwa kuendelea kuratibu

utekelezaji wa mipango itakayosaidia kupunguza madhara yanayoweza kujitokeza. Aidha,

sekta, mamlaka husika na Kamati za Usimamizi wa Maafa katika ngazi ya Mkoa, Wilaya,

Kata na Vijiji/Mitaa zinashauriwa kuchukua hatua stahiki ikiwemo kutoa elimu na miongozo

itakayohamasisha kuzuia au kupunguza madhara.

j) Vyombo vya Habari

Vyombo vya habari vinashauriwa kupata utabiri, kufuatilia na kusambaza taarifa na

tahadhari za hali ya hewa pamoja na zile zilizo huishwa na Mamlaka. Vyombo vya habari

pia vinashauriwa kutafuta na kutumia ushauri wa kisekta kutoka sekta husika wakati wa

kuandaa na kutoa taarifa mtambuka za hali ya hewa kwa jamii. Aidha, vyombo vya habari

vinashauriwa kuandaa na kusambaza makala za kitaalamu kwa kutumia lugha nyepesi kwa

lengo la kuhabarisha jamii juu ya matumizi sahihi ya utabiri wa hali ya hewa. Vilevile,

kushirikiana na wataalam wa sekta husika katika kuandaa vipindi maalum vya kutoa elimu

na kwa wakati kuhusu athari mbalimbali za hali ya hewa zinazotarajiwa kutokea na hatua

zinazopaswa kuchukuliwa ili kukabiliana na athari hizo.

Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania inawashauri watumiaji wa taarifa za hali ya hewa ikiwa

ni pamoja na wakulima, wafugaji, Mamlaka za Wanyamapori, Mamlaka za Maji na Afya

waendelee kutafuta, kupata na kuzingatia ushauri wa wataalamu katika sekta husika.

Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania itaendelea kufuatilia mwenendo wa mifumo ya hali ya

hewa na kutoa mirejesho ya mwelekeo wa mvua nchini kadri inavyohitajika. Aidha, wadau

wanashauriwa kuwasiliana na Mamlaka ili kupata taarifa mahsusi za utabiri wa msimu ili

kukidhi mahitaji maalum katika sekta zao.


Imetolewa: 31 Oktoba, 2023

Na: Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania

Comments