WANAWAKE WAPEWE NGUVU KUPITIA SANAA YA SARAKASI,WAONESHA UWEZO WAO
WANAWAKE WAPEWE NGUVU KUPITIA SANAA YA SARAKASI,WAONESHA UWEZO WAO
DAR ES SALAAM,
Mtandao wa Wasanii Wanawake nchini kwa kushirikiana na Chama cha Sarakasi Tanzania (TSA) pamoja na Makumbusho ya Taifa, umeendesha mradi wa kuwawezesha wasichana na wanawake kushiriki katika sanaa ya sarakasi na kupata fursa za kuonyesha vipaji vyao.
Mradi huo umejumuisha mafunzo na maonyesho yaliyofanyika kupitia programu ya Museum Art Explosion (MAE) katika Makumbusho ya Taifa na Nyumba ya Utamaduni jijini Dar es Salaam, ukiwa na lengo la kuongeza ushiriki wa wanawake katika sekta ya sanaa.
Wakizungumza katika maonyesho hayo, waandaaji wamesema mradi huo unalenga kuhakikisha wanawake na watoto wa kike wanapata nafasi ya kushiriki katika sanaa, uongozi na shughuli mbalimbali za kisanaa kwa usawa.
Amesema fursa hizo zinawezesha wasanii kuonyesha kazi zao, kuongeza ujuzi na kujenga nafasi zaidi za kiuchumi kupitia sanaa, huku akieleza kuwa Makumbusho ipo tayari kuwakaribisha wageni watakaofika nchini katika kipindi cha maandalizi na mashindano ya AFCON 2027.











Comments