SHIRIKA LA NYUMBU KIBAHA KUANZA KUZALISHA NGUZO ZA UMEME ZIZIZOPATA KUTU,LAJIVUNIA MWAKA MMOJA WA RAIS SAMIA.

 

SHIRIKA LA NYUMBU KIBAHA KUANZA KUZALISHA NGUZO ZA UMEME ZIZIZOPATA KUTU,LAJIVUNIA MWAKA MMOJA WA RAIS SAMIA.

Brigedia Jenerali Hashim Yusuf Komba ambaye pia ni Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Tanzania Automotive Technology Center (TACT),Kamanda wa Kikosi Cha Nyumbu Project kilichopo Wilayani Kibaha Mkoani

waandishi kutoka vyombo mbalimbali vya habari wakiendelea kupata maelekezo.

Mkurugenzi wa uzalishaji wa TATC, Meja Simon Rwegoshora akiwaonesha waandishi wa habari (hawapo pichani) gari la kuzimia moto katika uwanja wa ndege wa Dar es salaam ambalo linakarabatiwa na shirika hilo

Brigedia Jenerali Hashim Yusuf Komba ambaye pia ni Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Tanzania Automotive Technology Center (TACT),Kamanda wa Kikosi Cha Nyumbu Project kilichopo Wilayani Kibaha Mkoani

Mkurugenzi wa uzalishaji wa TATC, Meja Simon Rwegoshora akiwaonesha waandishi wa habari (hawapo pichani) gari la kuzimia moto katika uwanja wa ndege wa Dar es salaam ambalo linakarabatiwa na shirika hilo 

Shirika la Tanzania Automotive Technology Center  TATC-NYUMBU limesema liko katika hatua za kusimika mitambo mipya kwa ajili ya kuanza kuzalisha nguzo za umeme za chuma zizizopata kutu kufuatia serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan kulipatia shirika hilo kiasi cha shilingi bilioni 9 katika mwaka wa fedha 2021/22.

Akizungumza na waandishi wa Habari kutoka vyombo mbalimbali  vya habari waliotembelea shirika hilo ili kujionea utekelezaji wa majukumu yake,Mkurugenzi mkuu wa shirika hilo la TATC-Nyumbu,Brigedia Jenerali Hashim Komba amesema kuwa hayo yamejiri baada ya shirika kuandaa mpango mkakati wake wa kipindi cha miaka 10 ambao Rais Samia aliupitisha hivyo fedha hizo bilioni 9 ambapo bajeti yake ni bilioni 25  zimeasaidia shirika hilo katika Nyanja mbalimbali.

Ameongeza kuwa shirika la TATC-Nyumbu limeingia makubaliano na shirika la umeme Tanzania,Tanesco kuwajengea nguzo za umeme na vifaa vingine mbalimbali hivyo mitambo hiyo itakaposimikwa itaisadia serikali kupitia shirika hilo kutotumia fedha nyingi katika uagizaji wa nguzo hizo za umeme ambazo zitakuwa zinazalishwa hapa nchini.

Aidha ameongeza kuwa tangu kuanzishwa kwa shirika hilo ambapo mwaka 1977 ulianza kama mradi wa Nyumbu ambayo yalikuwa maono ya Baba wa Taifa na Rais wa kwanza wa Tanzania Hayati Julius Nyerere na baadaye December 14 mwaka 1984 ambapo lilibadilishwa kutoka kuwa mradi na kuwa shirika ambalo litasaidia katika kuendeleza ukuaji wa kiteknolojia hapa nchini kwa kufanya utafiti wa kiteknolojia kwa kuhuisha na kusanifu mitambo mbalimbali ambapo mpaka sasa pia shirika hilo lina mradi wa mtambo wa kusindika nyuzi za katani,mradi wa kutengeneza mkaa utokanao na taka za majumbani na udongo mfinyanzi ambao utasaidia katika utunzaji mazingira.

Ndugu waandishi wa habari ambao leo mmetutembelea shirika letu pia linazalisha vifaa mbalimbali vya shirika la maji la Dawasa na pia tumetengeneza mashine za kisasa za ubanguaji na uokaji wa korosho,sambamba na kutengeneza mashine ya kukamua juice ya ndizi na pia tumebuni gari la nyumbu ikiwemo la kubeba wanajeshi,maji na mchanga na pia tumetengeneza gari la kijeshi la kubeba deraya  la kimapigano ARV na tunendelea na usanifu ili kuwa na magari ya kibiashara na magari haya yataipunguzia serikali gharama za kuyaagiza nje ya nchi alisema Brigedia Jenerali Komba.

Hata hivyo shirika la TATC nyumbu pia lina mradi wa kutengeneza magari ya zimamoto ambapo tayari limeshayakarabati magari 11 kutokana na mkataba wao na jeshi la zimamoto na uokoaji  na sasa wanaendelea kuyaunda magari mapya matatu ambayo uundaji wake umefikia katika hatua nzuri.

Aidha majukumu ya shirika hilo pia kwa mujibu wa mkurugenzi wake Mkuu ni pamoja na kutoa ushauri wa kiuhandisi ambapo walitoa ushauri kwa benki kuu ya Tanzania BOT  katika ununuzi wa mashine ya kuhesabu pesa na tayari wameingia ushirikiano na shirika la maendeleo ya utafiti wa kilimo TARI ili kutengeneza mitambo ya kuchakata miwa ya wakulima ili kusaidia miwa yao isiharibike na upatikanaji wa uhakika wa sukari ambapo utafiti ili kuanza mradi huo unaendelea.

Hata hivyo Brigedia Jenerali Komba ameongeza kuwa shirika hilo limefanya usanifu wa vifaa mbalimbali ikiwemo kutengeneza breakblocks za shirika la reli Tanzania TRC,Uzalishaji wa vipuri katika sekta ya madini,vipuri vya magari na chemba za majitaka na pia hufanya ukaguzi wa mitambo inayonunuliwa na serikali kupitia wizara ya ulinzi na jeshi la kujenga Taifa ambayo ni mitambo ya kijeshi na pia hutoa huduma za kiufundi JWTZ na Dawasa na pia ndilo shirika lililobuni na kutengeneza mageti ya Ikulu ya Chamwino iliyopo jijini Dodoma na pia limefanikiwa kufanya utafiti wa teknolojia mbalimbali hapa nchini na linaunga mkono sera ya viwanda ya serikali ya awamu ya sita kwa kuanzisha viwanda mbalimbali ikiwemo cha misumari na tofali,huku likiitaja changamoto ya ukosefu wa fedha za niradi yake kulingana na uhitaji sambamba na utumiaji wa baadhi ya mitambo ambayo ni chakavu.

Aidha limeiomba serikali kupitia wizara ya ulinzi na jeshi la kujenga Taifa waendelee kutoa fedha za maendeleo ya shirika hilo huku likiwataka watanzania kuiendeleza amani waliyo nayo kwani ni tunu kubwa ya Taifa letu.


Nao baadhi ya waandishi waliotembelea shirika hilo akiwemo Judith Chao wa televisheni ya mtandaoni ya Spark TV ameishukuru wizara ya ulinzi kwa kufanikisha ziara hiyo ya wanahabari kutembelea shirika la Nyumbu na kuzitaka wizara nyingine kuwa na ziara kama hizo ili kuwajengea wanahabari uwezo wa kuziandika vyema habari katika Nyanja mbalimbali.

‘’kiukweli nilikuwa sifahamu zaidi kuhusu shirika hili zaidi ya kulisikia tu lakini leo nimetembelea na kuona mengi sana hasa uundaji wa magari na nimefarijika kuona gari aina ya Mac12 liliotengenezwa hapa nchini na tumeambiwa walianza kutengeza kuanzia toleo ya Mac 1 baada ya kuanzishwa kwa shirika hili hivyo sisi kama wanahabari tumejifunza mengi hapa na tutayaeleza kwa watanzania kupitia kazi yetu kama waandishi’’alisema Judith Chao wakati akizungumza na mtandao huu baada ya kumalizika kwa ziara hiyo ya wanahabari

 

 

Comments